Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba nichukue fursa hii kukupongeza tena, kwa jitihada zako na namna unavyosimamia Bunge letu. Lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu yao ya Wataalam kwa kutuletea hotuba nzuri, ambapo baada ya sisi wote kuchangia ninaamini kwamba tutakapoelekea kwenye Finance Bill yale mapendekezo ambayo Wabunge wengi wamependekeza, watayazingatia ili tuelekee huko sasa kufanya shughuli za maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niwapongeze sana Serikali kwa kutuletea Sheria ya Manunuzi, binafsi nimefarijika na ninajua hilo sasa litakuwa jambo ambalo litatusaidia wote. Niendelee kusisitiza kama wenzangu wote walivyosema suala la shilingi 50 kwenye maji. Lakini kwenye maji pia nigeomba niwapongeze kwa kuondoa gharama za dawa isitozwe kodi, pia ondoeni vile vifaa muhimu ambayo vya ku-filter maji ili na zenyewe katika hospitali zetu na sehemu za shule ambazo gharama yake ni kubwa ina import duty na VAT iondolewe ili watu wapate maji safi na salama. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia niendelee kuomba Serikali ihakikishe kwamba wafanye kwa hati ya dharura kuanzisha wakala wa maji. Fedha hizi mtazipata, anzisheni huo wakala ili ifanye kazi tunavyotarajia.
Ninaomba tena niwaombe Wizara ya Fedha wajaribu kuangalia suala la motor vehicle muiondoe. Hivi tunavyoenda sasa hivi kwa kukata kwa kupitia TRA wekeni kwenye mafuta, ili wale wanaokwepa wote wasiweze kukwepa. Ukiweka kwenye mafuta watayatumia mafuta atakuwa analipa na yule ambaye atumii atakuwa na gharama ndogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo mzima ulivyokaa, ukiweka kwenye mafuta itakuwa ina unafuu kwetu. Hata mambo ya uendeshaji wake na namna ya gharama za ku-print itapungua, itakuwa mtu akiweka mafuta ameshamaliza kila kitu. Lakini pia kwa wale ambao wako nje ya wigo wa hiyo kodi, wakiweka Serikali itakuwa inapata mara mbili ya hii mnayopata leo. Kwa nini wakati tukiwaelekeza mtapata mapato mnakwepa kuweka? Tunaomba huo ushauri mchukue, ili suala la motor vehicle lifanyiwe kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, niombe tena tuangalie namna ya kupata fedha ya uhakika ya utafiti na masuala ya mazingira. Leo hii hakuna dunia, haya mambo yote tunayosema tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda, bila utafiti ni hakuna kitu, na utafiti tumetenga fedha kidogo sana. Tuangalie namna ya kupata fedha za utafiti na suala la mazingira, kwa sababu mazingira pia ni muhimu sana huko tunakoelekea gharama tutakazotoza kuboresha hali ya mazingira itakuwa mara kumi ya hii ya leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, bBado kwenye suala la Sheria ya Finance Bill, mmeondoa msamaha kwenye vifaa vya natural gas lakini pia mimi ningependekeza ongezeni hata gesi ya kawaida liquid petroleum gas ili tuache kutumia mkaa, haya majiko na nini; ikiwa bei ni ndogo tutaacha kuharibu mazingira na pia itakuwa ni nafuu kwetu. Kwa hiyo, muondoe hizo kodi huwezi kupata kote kote. Huwezi ukapata kote kote, sehemu moja lazima upoteze nyingine upate. Kwa hiyo, kama mnapenda mazingira ondoeni hiyo kodi kwenye majiko.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ningeomba ni katika suala la EFD hii Electronic Fiscal Devices ndiyo njia pekee tutapa kodi yote tunayostahili kupata, leo hii mliahidi mtaleta mashine za kutosha, sijaona kwenye bajeti mashine za kutosha, naomba tulishawahi kupendekeza ruhusuni watu binafsi walete mradi vile viwango mnavyotaka zile specification wapeni. Mtu akiamua hapa Dodoma siyo lazima ununue mashine shilingi 700,000, mtu kama hizi decoders anaweza akakukodishia kila mwezi ukamlipa shilingi 30,000, shilingi 50,000 na service anakufanyia. Kwa hiyo muangalie mfikirie nje ya box, hili suala bila kuwa na EFD za kutosha mashine hizo 12,000 mnazosema hata Dar es Salaam peke yake Wilaya moja hazitoshi, kwa hiyo tukitaka kukusanya kodi zaidi hakikisheni suala la EFD mnalifanyia kazi kwa mapema sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine suala la formal sector na informal sector. Mfumo huu na hizi tozo za penalty mlizokuja nazo za kodi kwamba mtu akichelewa kidogo, penalt kila mwezi asilimia tano itafanya watu wengi zaidi warudi kwenye informal sector, teremsheni kodi, compliance iwe kubwa iwe tax friendly, watu walipe kodi vizuri zaidi, lakini hapa mnawatisha watu. Hivyo ningeomba sana hili suala la kwenye kodi tuliangalie vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo mzima wa kodi wetu bado haujakaa vizuri. Kwa mfano, leo bidhaa zile ambazo tunazalisha ndani ya nchi, mbolea, net ukiwa ndani ya nchi raw material yake inatozwa kodi na hawapati refund. Kwa zamani ilikuwa zero rated tumeondoa zero rated, aki-export hiyo bidhaa mbolea na net akipeleka tu Kenya anarudishiwa zile kodi zake, aki-import tena hiyo hiyo bidhaa akiirudisha hana kodi, sasa mtafanya watu wasizalishe ndani ya nchi bora mtu atoe nje na kurudisha ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo wetu wa kodi bado haujakaa sawa na ninaomba tu tuangalie la sivyo hii ndoto yetu ya kwenda kwenye viwanda, hatutafikia kama mfumo wetu wa kodi tusipouangalia vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza kwamba TRA iwe ni one stop center, kodi zote na zile tozo ambazo siyo za kodi zote zikusanywe na TRA, na pia ingeanzishwa huduma center, kila mtu ambaye anataka huduma mbalimbali kuna Wabunge hapa tena Mheshimiwa Makamba alishawahi kuisemea. Tuanzishe one stop center easy of doing business iwe vizuri, ikiwa hivi hata wale watu ambao wako nje ya wigo wa kodi labda anafanya biashara zingine lakini leseni yake akitakiwa kukatia TRA, huyu mtu atalipa angalau kidogo, na tutaweza kupata mapato yetu yote vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine tunaomba kwamba hizi kampuni za simu zote ziwe listed kwenye stock exchange. Kwa nini makampuni madogo yawe listed na haya ambayo wanafanya biashara kubwa hawawekwi humo. Ningeomba sana kampuni zote, ziwekwe humo, lakini muhimu kuliko yote, tufanye reseach na statistics hatutumii kabisa statistics na ndiyo maana hatuendi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo ni muhimu sana ni kwenye sekta ya kilimo. Sekta ya kilimo tuliahidiwa kwamba kodi nyingi na ambazo ni kero mngeziondoa kwa kweli mimi nilisikitika baada ya kuona kwamba kwenye Bodi ya Pamba mmeondoa shilingi laki nne na nusu hata mngeacha isingeleta tofauti yeyote. Hata hizo kodi kwenye angalau kwenye korosho mmejitahidi kuondoa asilimia kadhaa kwa mwaka mzima inaondoa kiasi fulani lakini hizi zingine na sekta yetu ya kilimo haitaweza kukua, kama tutakuwa tunaendelea na utitiri wa kodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ningeomba kwamba mngeunganisha Regulatory Board zote ziwe chini ya bodi moja iitwe Tanzania Regulatory Board na hizi zingine zote ziwe taasisi chini yake ili wanapoenda kufanya ukaguzi au wanapoenda kufanya shughuli mtu analipa mara moja basi, wale watu wanatakiwa kama ni sekta fulani wataalamu wa sekta hiyo kutokana na zile idara wataenda kwenye hiyo bodi, hata wafanyabiashara wataona kuna unafuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo machache niendelee kupongeza jitahaa hizi zilizopo, mindset change na nina uhakika kwamba tunaweza kufanikiwa Tanzania ya viwanda. Ahsante, hongereni sana.