Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kutoa pongezi kwa Waziri wa Fedha, Naibu na Wizara nzima ya Fedha kwa sababu wametengeneza bajeti ambayo ni ya mwaka mmoja lakini iko kwenye picha ya miaka mitano na iko kwenye picha ya dira yetu ya maendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyojadili hii bajeti usiichukue kama ni ya mwaka mmoja, lazima uone kwamba ni bajeti ambayo imeanza safari ya kwenda mwaka 2025. Kwa hiyo ikiwa kweli tumedhamiria kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 inamaanisha bajeti yetu lazima inapanuka, inakuwa kubwa na fedha nyingi zinaenda kwenye maendeleo na siyo matumizi ya kawaida na ndiyo shukrani zangu nazitoa kwenye hii bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesema tunataka kuwa nchi ya kipato cha kati mwaka 2025 maana yake ni kwamba ukipiga hesabu, bajeti yetu sasa hivi ni vizuri nikiongea kwenye dola kwa sababu nalinganisha na nchi zingine, GDP yetu (Pato la Taifa) karibu kwenye bilioni 55, 56. Kama tunataka kuwa nchi ya kipato cha kati, mwaka 2025 tunataka bajeti yetu ambayo itaonesha kwamba GDP per capita (pato la mtu mmoja) litakuwa la dola 3,000 inabidi tuizidishe mara nne. Kwa hiyo hii bajeti ni kubwa kwa sababu ifikapo mwaka 2025 tukiwa nchi ya kipato cha kati ni lazima tuwe na GDP ambayo ni zaidi ya bilioni 200 tuzidishe mara nne bajeti ya sasa hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa basi engines ziko nyingi sana, engine za kupeleka vitu huko mbele huko na engine mojawapo ni umeme, na ndiyo maana bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini imekuwa kubwa ni ya shilingi trilioni 1.23 katika hiyo bajeti asilimia 94 zinaenda kwenye maendeleo na ukichukua kwenye maendeleo asilimia 98 inaenda kwenye umeme. Hapo ndipo unajua bajeti ya Serikali iliyotayarishwa na Dkt. Mpango na wenzake imedhamiria kweli kutufikisha uko. Dalili za kusema kwamba fedha zinapatikana ni kweli zitapatikana, mwaka huu tunaomaliza mwezi huu, Wizara ya Nishati na Madini upande wa maedeleo tumeshapata asilimia 82 na REA - umeme vijijini tumeshapata asilimia 81.
Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti yetu kwa hiyo ni kwamba umeme vijijini ndiyo itawatoa watu kwenye umaskini. Bajeti mliyoipitisha ya umeme vijijini imo ndani ya bajeti kubwa ya Serikali ambayo ni ya umeme vijijini shilingi bilioni 534.4, hii imeongezwa kwa asilimia 50 ya bajeti ya mwaka uliopita. Lakini Waheshimiwa Wabunge na Watanzania ni kwamba kwa mara ya kwanza kwa historia ya nchii hii, na kuonesha hii Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kujenga nchi ya viwanda, ni kwamba umeme vijijini tutakuja kufikisha trilioni moja. Kwa sababu hii ni Serikali inayoaminika, hata wenzetu wanaopenda kutuchangia maendeleo na wao wanaweza wakachangia zaidi ya bilioni 500 na taarifa nitawapatia ndani ya wiki mbili kutoka sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hii bajeti inahakikisha umeme unapatikana, siyo umeme tu kusambaza, lakini hii bajeti ndiyo itatuhahakikishia kwamba vyanzo vyetu vyote tulivyonavyo vya umeme tunaanza kuzalisha umeme. Tumejipanga kuzalisha umeme kutokana na gesi asilia, makaa ya mawe, maji, sola, upepo, joto ardhi, mawimbi (tides and waves) na mabaki ya mimiea (bio energies). Hayo yote yako kwenye hii bajeti ya trilioni 29.5, kwa hiyo ndugu zangu Wabunge tusipoipitisha hii, tukiwa na wasiwasi nayo basi haya yote ya umeme hayatakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, na hii bajeti uzuri wake ndiyo inakuja kutuhakikishia kwa mara ya kwanza kwa historia ya nchi hii haya mambo ya umeme ambao unakatikakatika hii bajeti ndiyo nakuja kutoa suluhisho la kudumu. Tunajenga njia za kusafirisha umeme kutoka kilovoti 220 tunakwenda kilovoti 400.
Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge, mimi ningependa kuzidi kuwashawishi kwamba hii bajeti siyo ya mwaka mmoja bali inaanza safari ya kutufikisha mwaka 2025 na kwenye hii bajeti ndiyo tumeweka miradi mingi ya usambazaji wa umeme na ni muhimu sana. Waheshimiwa Wabunge wengi mmelalamika kwamba kuna vijiji vimerukwa. Hii bajeti ndiyo ina mradi wa kushusha transfoma na kusambaza nyaya kwenye vijiji ambavyo vimerukwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge, mmesema hii sekta ya nishati haijashikwa vizuri sana na Watanzania. Hii bajeti ndiyoina fedha za kuwawezesha wazalishaji wadogo wa umeme na wao waweze kuchangia kwenye umeme wa Gridi ya Taifa. Vilevile kwa upande wa kuboresha upatikanaji wa umeme, hii bajeti itatuwezesha kuibadilisha TANESCO kabisa itoke TANESCO ya zamani kuja TANESCO ya karne ya 21. TANESCO itakuwa na ushindani, lakini bajeti ya kubadilisha muundo, mfumo na utendaji unaolalamikiwa wa TANESCO uko kwenye hii bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaoenda huko kuanzia tarehe 1 Julai tunaweka taratibu za kisheria za kunyang‟anya TANESCO mamlaka ya yenyewe ndiyo inazalisha peke yake, ndiyo inauza umeme peke yake, ndiyo inasafirisha umeme peke yake.
Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge, mimi nigependa bado kusisitiza kwamba ni muhimu sana hii bajeti tukaiunga mkono na istoshe tumekuwa na sehemu tunaulizia ni kwamba kwa mfano wengine wamesema fedha za CAG, fedha za nani, ukweli ni kwamba bajeti hii acha ianze kufanya kazi na mahali ambapo tutakwama tutarudi tena hapa Bungeni kurekebisha.
Meshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge, kwa hiyo hii bajeti ni muhimu na diyo itatufikisha mwaka 2025 ambapo GDP per capita yetu ambayo itatoka sasa hivi dola 945 GDP per capita mpaka kwenda dola 3,000 kama GDP per capital.