Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Udhibiti wa Matumizi ya Dawa na Mbinu za Kuongeza Nguvu Michezoni

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Udhibiti wa Matumizi ya Dawa na Mbinu za Kuongeza Nguvu Michezoni

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa napenda kutoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri wa Michezo kwa kuleta Azimio hili hapa Bungeni. Napenda kusema kwamba tumechelewa sheria hii ilitakiwa tuipitishe mapema kwa sababu wachezaji wetu ndiyo waathirika wakubwa wa matumizi ya madawa haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ningependa kusisitiza pamoja na kwamba tunapitisha hili Azimio naungana na Serikali kwa maamuzi haya kwa asilimia mia moja kwamba tupitishe. Matumizi ya madawa haya ya kuongeza nguvu hayatofautiani kabisa na upangaji wa matokeo. Upangaji wa matokeo unasababishwa na mambo mengi. Kwanza watu wanapanga matokeo kwa maana ya kuangalia zile award zinazotolewa kwenye michezo. Nchi ambazo zimeendelea zimekuwa ni za kwanza kuathirika na matumizi haya kwa sababu ya kutaka kupanga matokeo, walikuwa wanapanga matokeo ili watu waweze kuneemeka kifedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukitazama sasa hivi ni kwamba idara ya michezo yaani ndiyo inayolipa zaidi, ukitaka kuwa na kijana ambaye anaweza akaleta kipato kikubwa ni yule kijana anayecheza mpira kwa mfano au wanaokimbia riadha. Wale wanapewa kipato kikubwa sana na kipato hiki ndicho inakuwa ni motivation yaani inasabisha watu kutumia madawa ili kuweza kupanga matokeo. Kwa hiyo, matokeo yanapangwa mtu anapata ushindi usio wa halali, anapata ushindi ili aweze kujilimbikizia pesa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hii tunasema kwa Tanzania tulichelewa ilitakiwa tuwe tumeanza na watu wakajifunza na wakaelewa kwa ufasaha. Ni toka zamani ukiangalia mwaka 1968 Olympic ndiyo walianzisha lakini lilikuwa ni tatizo la muda mrefu, watu walikuwa wanatumia hata vyakula vingine vya kawaida ili aweze kuongeza nguvu waweze kupata performance kubwa katika michezo. Kulikuwa kuna uyoga ulikuwa unaitwa ni hallucinogenic mushroom, ilikuwa ni mushroom maalum kwa kuongeza nguvu. Watu walikuwa wanatumia hata hizi mbegu za ufuta ili waweze kuongeza performance waweze kupata kipato.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, kwa pamoja hapa napenda kusema kwamba, nashukuru sana hii sheria imeletwa tuipitishe, tuipitishe kwa maana ya kwamba tuungane na Umoja wa Kimataifa UNESCO, kwa maana ya kwamba Tanzania nayo itambulike ni nchi inayopingana na haya madawa ya kuongeza nguvu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tungekwenda mbali zaidi, tukiangalia kuna matumizi ya pombe, matumizi ya bangi. Tunashukuru Serikali inapambana na matumizi ya bangi, kwa kweli kuna vita vikubwa vinavyoendelea na masuala haya ya cocaine na vitu vingine. Tunashukuru Serikali inafanya kazi vizuri kupambana, lakini kuna tatizo la viroba! Viroba na lenyewe ni tatizo kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tungeangalia namna ya kupiga marufuku viroba; viroba vipigwe marufuku kwa sababu na vyenyewe ni tatizo kubwa, kuna vijana wengi wanaathirika na viroba wanashindwa kucheza, wanastua kidogo kwa maana ya kuongeza nguvu lakini baada ya muda wana develop kwenye addiction, tunaharibu nguvu kazi ya Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli vijana ni wengi, nimezunguka baadhi ya maeneo tulikuta watu wanatumia viroba kwa kweli inasikitisha, viroba vinatumika sijui kwa sababu ni cheap, sijui ile packing iko flexible mtu ananunua anatia mfukoni, ni rahisi kununua kwenye vibanda, kwenye vioski vinauzwa viroba. Ukitazama watu wanatumia viroba kabla hawajaingia kucheza mpira au kukimbia riadha mtu anastua kidogo, anasema anaongeza nguvu, lakini baada ya muda anakwenda kwenye drug dependence au alcohol dependence, ana-develop addiction. Kwa hiyo, tunaomba Serikali nayo itazame kwenye viroba tupunguze matumizi ya viroba. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ningependa kuongelea, kwa sababu tunaongelea upangaji wa matokeo, kutumia hizi nguvu za ziada ni kwamba unapanga matokeo kwamba unakwenda kushinda. Kuna tatizo Mheshimiwa Waziri la rushwa kwenye michezo na lenyewe linapanga matokeo. Unakuta ma-referee kwenye mpira wa miguu wanapewa pesa ili kuweza kupanga matokeo, ina-demoralize kabisa. Ukienda kuangalia mpira unakuta refa akishapewa mlungula pasipokuwa na penalty yeye anatoa penalty, pasipokuwa na offside yeye anazuia kuna offside. Kwa kweli ina-discourage watu kucheza mpira, hata watazamaji ina-discourage kwa maana unaangalia wakati matokeo yameshapangwa, timu zetu kubwa Simba na Yanga zinashiriki kwenye kupanga matokeo, wachezaji wanapewa rushwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuangalie ni namna gani ya kutengeneza sheria kuweza kuhakikisha kwamba tunaondoa kwa sababu upangaji wa matokeo kwa kweli ni tatizo na tulishasema mpira au michezo ni afya, michezo ni uchumi, michezo ni burudani. Kwa hiyo, tuangalie uhalisia wa michezo, tuilete michezo katika hali yake halisi. Mtu ashiriki ashinde kwa halali kama ni mkimbiaji wa riadha aweze kushiriki kwa halali. Tunaomba muangalie hayo mambo matatu ambayo ni viroba, rushwa na hili Azimio tulipitishe kwa faida ya Taifa letu na kwa dunia nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.