Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa fursa niweze kuchangia. Naomba nianze kwa kuunga mkono hoja na vilevile kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na uongozi wa Wizara kwa hotuba nzuri ya bajeti ya Wizara yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mawili, matatu niongee kwa haraka haraka. Nianze na mchango wa Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka ambao ni mchango mzuri. Sisi kama Serikali tunaheshimu sana constructive criticism. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameongelea kuhusu Wabunge wa EALA kwamba hawana ofisi. Nataka kusisitiza tu kwamba tofauti na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki sisi ndiyo wenyeji, sisi ndiyo tume-provide headquarters ya EAC. Kwa hiyo, kiti chetu sisi kiko Arusha, ndiyo sehemu kuu ya East African Community na pale Wabunge wote wana ofisi zao. Tulitaka Wabunge wa EALA wawe na ofisi Dodoma sijui wakifanya nini, wawe na ofisi Dar es Salaam wakifanya nini? La msingi tukubaliane kwamba tuimarishe ofisi zao za Arusha waweze kukaa pale kwa ajili ya kufanya research zao na kutuwakilisha vizuri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, niongelee kuhusu mchango wa Mheshimiwa Hamidu Hassan Bobali kuwa Kenya na wenzetu wana Wizara mahsusi kwa ajili ya Afrika Mashariki. Nafikiri hapa tuongozwe na Treaty. Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ukiangalia Ibara ya 8(3)(a) inasema kwamba:-
“Each partner state shall designate a Ministry for East African affairs”.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ita-designate ina maana ita-appoint (itateua). Haisemi kwamba itakuwa na a Ministry exclusive for East African affairs. Hata ukiangalia Article 13(a), inahusu chombo cha juu cha maamuzi cha community, The Council of Ministers, kinasema:-
“The Council shall consist of the Minister responsible for East African Community affairs. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni Wizara ambayo imekuwa designated, ni Wizara imekuwa entrusted kubeba masuala ya East Africa. Hata Serikali ya Kenya walivyoanza chini ya Mheshimiwa Rais Kenyatta walikuwa na Wizara ya Biashara, Utalii na Jumuiya ya Afrika Mashariki na mimi wakati huo nilikuwa East Africa na juzi tu wamebadilisha sasa ni Wizara ya Kazi na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Unaangalia mwenyewe strategic interests za nchi yako ufanyeje! Hata unaweza kuamua kuwa na Wizara ya Ulinzi na Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa sababu hili ni suala tu ku-entrust Wizara yeyote iweze kui-house hiyo community. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine ambalo napenda niliongelee kidogo, ni hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani ukurasa wa sita na wa saba. Kama nilivyosema sisi tunaheshimu sana constructive criticism, hatuna tatizo kwa uhuru walionao, wameongea haya, lakini lazima tuweke record sawasawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema kwamba amefanya uchunguzi ambao unaonesha kuwa chini ya Serikali ya CCM Ubalozi unatolewa kama zawadi kwa Makada walioisaidia kwenye kampeni, kwa Makada wa CCM wasiojua kitu kuhusu diplomasia ya uchumi ndiyo wanaokabidhiwa dhamana ya kuhakikisha Tanzania ifanikiwe kimataifa, wengi wao wangeweza kuwa Mabalozi wazuri sana wa nyumba kumi kumi lakini siyo kuwa Mabalozi wa nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliona kwamba hili tuliweke vizuri tu, naomba nisisitize kwamba tangu uhuru, viongozi wetu wamejitahidi sana kuwa waangalifu kuteua wanaotuwakilisha nje ya nchi. Ushahidi upo kwamba Mabalozi wetu wanapokuwa nje huko, Jumuiya ya Kimataifa inawaona, inawapa majukumu makubwa zaidi na siyo juzi tu, tumeanza toka kipindi cha Mwalimu Nyerere. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wengine wadogo hapa ngoja niwakumbushe. Tulikuwa na Kada wa CCM, Mzee Daudi Mwakawago alikuwa Katibu Mtendaji wa CCM, akapewa Ubalozi. Cha msingi hapa jamani ni kitabu, jamaa alikuwa amepiga kitabu vizuri hadi Kofi Annan akamuona pamoja na Ubalozi wake akamteua kuwa Mwakilishi wa Kofi Annan Sierra Leone na Mkuu wa UN Mission kule. Yote haya yanaonesha kuwa kitabu ndiyo kitu cha kwanza kinachotuongoza sisi kuteua Mabalozi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yupo Balozi James Kateka kama mmewahi kumsikia, ni judge wa International Tribunal for the Law of the Sea huko Humburg. Yeye ndiyo Mtanzania wa kwanza kuingia International Law Commission amekaa kule 10 years. Huwezi ukasema ana-qualification za nyumba kumi kumi.
Balozi Dkt. Asha Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Nitolee mfano wa Balozi mmoja ambaye hafai.
Mimi naomba Wapinzani muwe wavumilivu! Ninyi mkisema sisi tunakaa kimya, mbona utamaduni huo hamna? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Balozi Profesa Costa Ricky Mahalu, mimi naenda kufanya Uzanifu Ujerumani nimemkuta anawafundisha Wajerumani pale international law. Hawa ndiyo Mabalozi wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Balozi Kagasheki alikuwa hapa hapa, nimemkuta mimi Geneva akiwa Deputy Secretary General wa World Intellectual Property Organization. Tunajua kuteua watu! Balozi Dkt. Agustine Mahiga jamani huyo ana-record iliyotukuka, ameshakuwa Rais wa Baraza la Umoja wa Mataifa. Bila shule huwezi kuwa Rais UN utajiminyaminya tu midomo tu hovyo! Ameshakuwa mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Somalia na amefanya kazi iliyotukuka kule. Hawa ndiyo Mabalozi wetu wanaoteuliwa na Serikali ya CCM. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Balozi Getrude Mongela, Spika wa Bunge la Afrika; Balozi Juma Mwapachu, Katibu Mkuu EAC; Balozi Ally Mchumo, Mkurugenzi Mtendaji Mfuko wa Pamoja wa Mazao Brussels na wengine wengi wenye sifa nyingi. Wengine wana sifa zilizotukuka, mchukulie Balozi Ally Hassan Mwinyi nimuelezee nini? Balozi Salim Ahmed Salim nimuelezee nini? Balozi Benjamin Mkapa, naona niishie tu hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kusema taarifa ya Kambi ya Upinzani imejitahidi kwa kurasa nyingi kutuchora kama Serikali isiyo serious, non serious government! Wakisikia wanachama wa East Africa kwamba tunaitwa Serikali isiyo serious watashangaa kweli kweli kwa sababu sisi tumekuwa critical na ndiyo sababu Rais aliyepita Mheshimiwa Kikwete amekuwa Mwenyekiti kwa mwaka mzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Uenyekiti tunaenda kwa rotation basis lakini haikuwa accident alipoingia Rais mpya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli viongozi wa East Africa wakasema mzee tunaomba uendelee wewe mwenyewe kuwa Mwenyekiti, it is unprecedented! Ni kwa sababu we have a critical role katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi sisi tumefanya mambo mengi East Africa. Niwakumbushe machache tu, sisi ndiyo tumesimamia mchakato mzima wa admission ya South Sudan tukiwa Wenyekiti wa Jumuiya na mimi wakati huo nikiwa Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki. Siku hiyo tumekesha mpaka saa tisa kuweza kutengeneza proposal kwenda Summit kwa ajili ya admission ya South Sudan. East Africa inatambua mchango wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mungu kampa macho makini Mheshimiwa Rais kwa kugundua nyota ya Tanzania na kumfanya Waziri wa hii Wizara Mheshimiwa Dkt. Mahiga, he is a jewel, lazima tujivunie hapa. Sisi Watanzania tumesimamia mchakato wa kuishawishi Serikali ya Marekani kurefusha ule mpango wa AGOA wa kuuza bidhaa kwenye soko la Marekani bila kulipia ushuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niliongoza ile delegation ya Mawaziri wa East Africa tumekwenda Marekani ku-negotiate na Serikali ya Marekani na interests za Tanzania zilikuwa mbele sana. Lengo letu kubwa lilikuwa ni kwamba tuki-extend AGOA Watanzania tu-play a much more meaningful role katika biashara hiyo. Ndiyo maana tukaishia ku-sign the Cooperation Agreement on Trade Facilitation, Sanitary and Phytosanitary Measures and Technical Barriers to Trade.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba utatusaidia zaidi Tanzania kuliko nchi nyingine, tuliweza kuwa-convice wenzetu kwa sababu sisi Tanzania kinachotuangusha sana ni packaging, umaliziaji wa bidhaa zetu hivyo hatuwezi ku-penetrate kwenye masoko makubwa. Wenzetu Kenya sasa hivi wamechukua mpaka biashara zetu kwa sababu wao hata vitunguu wanajua namna ya kuvikata, kuvihifadhi na kukidhi zile sanitary measures na kuweza kupeleka kwenye masoko ya nje. Chini ya mkataba huu, Wamarekani wamekubali ku-extend hiyo technical service kwetu hapa na sasa hivi tumeongea na Mheshimiwa Waziri wa Biashara amelivalia njuga suala hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nirudie kusema naunga mkono hoja na namtakia Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kazi njema katika kuijenga nchi yetu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.