Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachangia kwa maandishi bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kuboresha majengo ya ofisi zetu za Balozi za Tanzania nje ya nchi, zinatia aibu kwa majengo kuwa machakavu hata rangi hayabadilishwi. Naishauri Serikali, pale ambapo baadhi ya nchi zinatupatia viwanja kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya kudumu ya Ubalozi mfano Oman, tuyajenge haraka iwezekanavyo ili kuepuka kunyang‟anywa viwanja hivyo na kupewa nchi nyingine kama ilivyotokea Oman; kiwanja chetu kupewa nchi ya India ambayo tayari wameshajenga jengo la kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mafungu ya fedha yapelekwe mapema katika Balozi zetu za nje ili kuboresha utendaji bila kusahau kuboresha mishahara na elimu zao na kuwashughulikia Watanzania wanaofanya kazi nje ya nchi ambao wanapata matatizo katika ajira zao au shughuli mbalimbali za kimaisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamekuwepo na tatizo la vyeti vya baadhi ya vyuo vyetu (certificates) kutotambulika katika nchi za nje, hali ambayo inasababisha usumbufu katika ajira kwa Watanzania waliopo nje. Mfano, Dar es Salaam Maritime Institute Certificates, hazitambuliwi Kimataifa kwa mujibu wa taarifa nilizopata toka kwa Watanzania, mabaharia wanaofanya kazi katika nchi za ng‟ambo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali ihakikishe inavitangaza vyuo vyetu Kimataifa kwa kufuata taratibu za Kimataifa ili vitambulike katika medani za Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali yetu kufanya taratibu ya kuondoa visa na kutumia entry katika nchi za Nordic United Arab Emirates, United Kingdom, German and Northern America. Hii itasaidia Watanzania wengi kupata fursa za kibiashara na kielimu, hali itakayowezesha Watanzania wengi pia kupata ajira na wale wenye vipaji vya michezo mbalimbali. Pia wataweza kuionesha dunia kuwa Watanzania wanaweza na wao pia watapata ajira. Mfano, wachezaji wa basketball, football, golf, tennis, athletics na kadhalika.