Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni nzuri na inaeleweka vizuri. Napongeza utendaji wa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu kwa kazi nzuri wanayofanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mwenyekiti wa Kamati, Makamu Mwenyekiti kwa kuishauri vizuri Serikali. Naomba ushauri wa Kamati uzingatiwe kwa maslahi ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ushauri; Ofisi zetu za ubalozi na maafisa wetu wasaidie katika kuutangaza utalii wa Tanzania. Wasaidie katika kuleta wawekezaji nchini mwetu na mkazo uwe kwenye ujenzi wa viwanda. Serikali iboreshe ofisi zetu za ubalozi kwa kuweka vitendea kazi vya kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika utendaji wa Soko la Pamoja la Afrika Mashariki. Elimu iendelee kutolewa kwa Watanzania. Serikali iweke mpango mkakati wa kuwatambua wanafunzi wetu wanaosoma nje ili kupunguza matatizo ya udhalilishwaji wa wanafunzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafunzi wengi wanakwenda kusoma nchi za nje bila utaratibu. Wanafunzi wanaosoma nje bila kuthibitishwa na TCU kwa nini wao hatuwaingizi kwenye ajira za moja kwa moja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuangalie kwa kuwa watoto wale ni Watanzania wanakwenda kuchukua ujuzi wa Mataifa mengine si kwa wote lakini wengine tuwape nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.