Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hamoud Abuu Jumaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HAMOUD A. JUMAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nichuke fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kuniwezesha kusimama kwenye Bunge lako Tukufu kwa mara nyingine, lakini pia niwashukuru wananchi wangu kwa sababu ndio ninasimama kwa mara ya kwanza, kwa kunirejesha tena bungeni kwa kipindi cha pili.
Vilevile nichukue fursa hii kukupongeza wewe kwa kazi kubwa ambayo unayoifanya hapa bungeni, waswahili wanasema; kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi; lakini wanasema raha tele, taabu ya nini? Lakini pia wanasema kwa nini uminyane na ukuta wakati malango upo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza nichukue fursa hii na mimi niipongeze Serikali kwa maana ya Waziri, Naibu Waziri na wataalam wake wote kwa kuandaa bajeti nzuri yenye lengo kubwa la kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2016 na hii imeonesha ushahidi hata katika kutenga bajeti ya maendeleo kwa mara ya kwanza tumetenga bajeti takribani asilimia 40. Hii yote inaonesha dalili njema ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Naamini fedha hizi zikienda vizuri na tukisimamia vizuri sisi Wabunge tunaweza tukafanya mambo makubwa zaidi, na hatimaye tukaleta maendeleo makubwa; na baadaye katika uchaguzi wa mwaka 2020/2025 tukapata kura nyingi na Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi upo uwezekano mkubwa wa kuendelea kushika dola. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ningependa kuchangia katika suala zima la mabasi ya mwendokasi, lakini vile vile niipongeze Serikali kwa kuanzisha mpango huu wa mabasi ya mwendokasi japo kuwa ziko changamoto mbalimbali ambazo zinajitokeza na sisi wote mashahidi, lakini niseme tu jambo hili zuri na nichukue fursa hii kumpongeza Waziri Mkuu na wote mashahidi tumeona amekwenda kupanda basi lile, Makamu wa Rais, Rais Mstaafu, ni jambo jema na ndio maana wanatamani na watu wengine waweze kwenda kupanda mabasi. Ziko changamoto mbalimbali, sisi wote mashahidi tunaona, kuna watu mbalimbali ambao wanavunja sheria, magari yanaigia katika njia ile ambayo hayaruhusiwi. Sasa ushauri wangu tuangalie Serikali ni jinsi gani ya kutunga sheria nyingine kali zaidi ili kusiingie tena na uharibu ambao mradi huu umeingia gharama kubwa na tumetumia pesa nyingi sana katika kuutekeleza mradi huu.
Lipo jambo lingine ninaloshauri, maana ya mabasi ya kwenda kasi, tungetafuta utaratibu, kwa mfano tungeanzisha basi lingine au mawili, matatu basi moja linatoka Kimara, linakwenda mpaka Posta, na lingine linatoka Posta mpaka Kimara. Pale Italy ipo moja treni inaitwa rapido ni treni ambayo inakwenda kwa spidi, sasa tukianzisha mabasi haya ya kwenda kasi mawili ili watu waweze kwenda kwa haraka zaidi, hata tukiongeza gharama kidogo itasaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tusiishie hapo, mabasi yale sasa hivi yamesaidi kwa kiasi kikubwa kupunguza foleni Dar es Salaam na sisi wote mashahidi. Tungeanzisha kujenga hata yard pale moja ya kuegesha magari, kuna watu wanatoka maeneo mbalimbali, inawezekana wakaja pale wakaegesha magari yao, na baadaye wakapanda mabasi wakaenda Posta, mjini wakafanya shghuli zao na baadae wakarudi katika shughuli hizi za kawaida. Ili twende vizuri zaidi, Serikali ilikuwa na mpango wa kujenga barabara ya njia sita kutoka Dar es Salaam kwenda mpaka Chalinze na baadaye kuelekea Morogoro. Naishauri mpango huu ufanywe haraka ziaidi tukijenga barabara ya njia sita itatusaidia sana kupunguza foleni. Kwa sababu leo ukitokea Dodoma, Morogoro na kuelekea Dar es Salaam ukifika Kibaha hapo katikati kuna kuwa na foleni kubwa. Kwa hiyo, tukijenga barabara ya njia sita itapunguza kwa kiasi kikubwa foleni za magari ili tuende vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, liko suala limezungumziwa sana na wenzangu suala la zima la CAG. CAG ameomba karibuni takribani shilingi bilioni 88 lakini pesa aliyopewa takribani shilingi bilioni 44; pesa hizi ndogo sana, nashauri na wenzangu wengi wamelizungumzia kwa kasi kubwa, naomba tu Serikali iangalie ni jinsi gani ya kuongeza fedha hizi kwa CAG ili tuweze kufanya kazi vizuri. Kwa sababu huyu ndio mwangalizi wetu akipata fedha ndogo hizi atashindwa kufanyakazi yake vizuri, kwa hiyo, naomba aweze kupata pesa hizo ziweze kwenda vizuri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namba tu ni-declare interest mimi na Mheshimiwa Zungu wavaaji wazuri sana wa mitumba, sasa katika eneo hili naona mmeongeza kodi kubwa ya mitumba…
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante.