Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwanza nimshukuru Mungu kwa kupata hii nafasi, lakini pia naomba kuchukua nafasi hii nikupongeze Mheshimiwa Naibu Spika, kwa uimara na tunaomba Mungu aendelee kukujalia kwa afya njema ili uendelee kukalia hicho kiti na kusimamia kanuni na sheria mbalimbali na Chama cha Mapinduzi hakikufanya kosa kukupendekeza kwa kuwa hiyo ni fani yako na unaitendea haki.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niipongeze bajeti, ni bajeti nzuri ina muelekeo mzuri kwa kuongeza pande wa Maendeleo na tumefikia asilimia 40 na vilevile imezidi kwa trilioni saba bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016; kwa hiyo tunategemea kupata mambo mazuri.
Pamoja na kuiunga mkono bajeti kuna mambo machache ambayo ningependa kuchangia na zaidi nianze na suala la kodi kwenye masuala ya Wabunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, binafsi siungi mkono hii hoja ya kuondoa msamaha kwa Wabunge kwa sababu Serikali iliangalia kwa mantiki kabisa mwaka ambao iliweza kuwapa Wabunge na viongozi wengine msamaha wa kodi waliona kuna maana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiangalia kwa mujibu wa Katiba wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wabunge ndio chombo kikubwa katika Jamhuri ambacho kina wajibu wa kusimamia na kuishauri Serikali. Kwa hiyo, na tuko hapa kwa niaba ya wananchi, kwa hiyo unapomuongezea gharama Mbunge ni sawa na unamuongezea gharama mwananchi. Kwa hiyo, tunaomba sana sasa Serikali tuko kwenye hiki chombo, tunaisimamia Serikali; kwa hiyo, tunaomba hili kusudio liweze kuondolewa maana kupitisha haya marekebisho ya hii sheria ni sawa na mtu umepanda kwenye mti unakata tawi ambalo umekalia mwenyewe, sasa sidhani kama Wabunge tutaweza kuiunga mkono hoja hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kwenye kodi (Capital Gain Tax) kwenye mambo ya hisa, Serikali tuna soko la hisa na moja ya faida kubwa ya kuwa na soko la hisa ni kuweka uwazi katika makampuni ambayo yameingia pale, na makampuni ambayo yako pale kwenye soko la hisa yanatoa mahesabu yao kwa uwazi, utendaji wao wa kazi. Kwa hiyo, wananchama ambao ndiyo wale wenye hisa wakati wa kuuza zile share zao kuna faida wanayoipata kwa utofauti wa bei ya kununua na kuuza. Sasa kwa kusudio la Serikali kutoza kodi liangalie suala zima la kwamba tuhamasishe uwekezaji.
Kwa hiyo, niishauri Serikali tuangalie namna ambayo ya kutoza kodi kwenye hii faida mtu anapouza zile hisa zake ambayo itakuwa inaudhibiti mzuri. Ukichukua mtu amenunua share mwaka mmoja uliopita amekuja ameuza leo sasa ile bei aliyonunulia kumbukumbu nani anakuwa ameitunza?
Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri ningeshauri kwamba kwa sasa hivi share zikiuzwa inachukuliwa asilimia mbili ambapo broker anapata asilimia yake, soko la hisa linapata na capital market wanapata mgao wao. Sasa Serikali iangalie namna kwenye hii asilimia mbili tuongeze labda tupeleke asilimia tatu, asilimia moja ndiyo iwe kipato ambacho kinaenda kuingia upande wa Serikali badala ya kuweka kodi ambayo kui-manage kwake itakuwa inasumbua.
Mheshimiwa Naibu Spika, uzuri mkubwa katika watu ambao wapo kwenye masoko ya hisa wanatuwezesha kuongeza ufanisi, natoa makampuni zaidi ya 20 hatujafikia wenzetu kama Wakenya wana makampuni 62. Kwa hiyo, tuhamasishe makampuni mengi zaidi yaweze kuingia kwenye Soko la Hisa ili kuwe na utandawazi na Serikali iweze kukusanya kodi zake zote ipasavyo. Kwa hiyo, tutaomba sana Serikali namna ya kutoza hapa tuongeze asilimia hii mbili inayotozwa sasa hivi badala ya kuangalia kodi ambayo itakuwa kui-manage kwake pale itakuwa ni kazi ngumu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumezungumzia kuondoa au kufuta baadhi ya tozo kwenye mazao ya kilimo. Tunaomba Serikali iangalie kwa umakini kwa sababu kuna maeneo ambayo Halmashauri zetu ndipo wanapopatia kodi. Lakini vilevile kuna kodi na tozo ambazo haziingii kwenye Serikali au kwenye hizi Halmashauri zinaenda kwenye Vyama vya Msingi na wakulima wamekuwa wakilalamikia sana. Kwa hiyo, ninaunga mkono kuondoa zile kodi ambazo hazina tija zinaongeza gharama kwa wakulima na hasa zinakuwa zinafaidisha tu vyama vya msingi na makampuni mengine ambayo yananunua hayo mazao ya biashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini zaidi ya hapo tungependa kwamba katika hotuba ya Waziri hatukuona upande wa tumbaku kwamba ameweka ni tozo zipi ambazo zinapendekezwa kuondolewa. Wakati Wabunge tumeshazungumzia sana kwenye upande wa tumbaku kuna gharama nyingi, wakulima wanapata taabu kwenye bei na hizo tozo mbalimbali, kwa hiyo tunaomba ziweze kuangaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni suala la maji, sera ya maji ilianza mwaka 1991 ikafeli, 2002 ikaboreshwa lakini ukiangalia mtiririko wa bajeti upande wa maji ndiyo una asilimia ndogo sana.
Kwa hiyo, nashauri angalau tuweke kati ya shilingi 20 kwa lita mpaka 50 ili tuweze kupata nakuunda mfuko wa maji tuweze kuboresha maji zaidi kwa wananchi ambao wengi wanakuwa na tabu kwenye kupata huduma ya maji na sera ya maji vijijini bado haijafikiwa ukamilifu wa zile mita 400.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la VAT kwenye upande wa Bima, Serikali inakusudia kuondoa VAT kwenye Bima upande wa ndege, lakini tujaribu kuangalia ni soko ambalo halina ushindani na je, kuondoka kwake kuondoa huu msamaha kuondoa VAT kwenye hizi bima upande wa ndege tunaathiri vipi mapato yetu na ni soko ambalo halina ushindani kwa hiyo, tutakuwa hatuna kwamba tunavutia zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitoa fedha na cealing kwa Halmashauri zetu, lakini tuombe mwaka ujao wa fedha Halmashauri ziangalie bajeti zao tukiangalia kiutawala Halmashauri ndizo zenye wajibu mkubwa wa kusimamia huko chini kwa sekta zote, lakini wanapangiwa kiasi kidogo kwa hiyo upande wa maendeleo kwa Halmashauri ambao ndiyo tunaangalia wapi tuna mapendekezo zaidi tunakuwa tunazuiwa na ukomo wa bajeti. Kwa hiyo, niombe Mheshimiwa Waziri Halmashauri zetu kwa mwaka ujao wa fedha ziweze kuangaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru naunga mkono hoja.