Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia Bajeti ya Serikali. Nianze kwa kukupongeza Mheshimiwa Naibu Spika kwa kazi nzuri unayoifanya ya kuendelea kuliongoza Bunge letu Tukufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango na Naibu Waziri kwa maandalizi mazuri ya bajeti na Serikali kwa ujumla. Pamoja na maandalizi haya mazuri, mapungufu hayakosi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza nianze na bajeti ya sekta ya kilimo iliyotengwa, asilimia nne nukta tisa ambayo ni takribani shilingi trilioni moja nukta tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninatamani sana malengo yetu ya Serikali na nchi yetu ya kuwa nchi yenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 tuyafikie na natamani sana malengo ya nchi yetu ya kuwa na uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2020 tuyafikie. Lakini ili tuweze kuyafikia, lazima tutende kwa vitendo, asilimia 4.9 ya bajeti ya sekta ya kilimo ni ndogo sana. Kwa sababu ukiangalia Watanzania walio wengi takribani zaidi ya asilimia 75 wamejikita kwenye shughuli za kilimo na hili tuweze kuwa na social economic transformation ya kuweza kutupatia uchumi wa viwanda, inatubidi kuhakikisha shughuli zao ambazo wanazifanya ndipo tuelekeze hizi sera za uchumi wa viwanda. Sasa shilingi trilioni 1.5 ni ndogo sana kama kweli tuna dhamira ya kujenga uchumi wa viwanda ambao unawagusa asilimia zaidi ya 75 ya Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango anaweza akasema kwamba tukisaidia kujenga miundombinu in one way or another tutakuwa tumesaidia sekta ya kilimo. Ni sahihi, miundombinu ni catalyst ya maendeleo, lakini ifike mahali turudi kwenye kutimiza lengo tulilosaini la Maazimio ya Maputo kwamba asilimia kumi ya bajeti iende kwenye sekta ya kilimo, bado tuko mbali sana. Nipende kuiomba Serikali jambo hili ilitilie maanani sana kwa sababu uchumi wa viwanda utakaowagusa Watanzania wengi, lazima tuhakikishe sekta ya kilimo tunajikita huko kuchakata kwa mazao ya wakulima na wafugaji ndio iwe focus ya mwelekeo wa Serikali ya viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili naomba nizungumzie bei ya kahawa. Waheshimiwa Wabunge wanaotoka kwenye Majimbo yanayolima Kahawa wameizungumza sana, viongozi kabla ya uchaguzi wamewaahidi wakulima wa kahawa kwamba zile kodi kero 26 zitaondolewa baada ya hii Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani.
Sasa nipende kumuomba Waziri wa Fedha atakaposimama kufanya wrap-up atuambie hizi kodi zinakatwa lini. Sasa hivi wakulima wa kahawa wako wanavuna kahawa, walitegemea bei ya msimu huu ihusishe makato haya ili wapate faida zaidi hata kama soko la bei ya kahawa la dunia liko chini, tukiondoa hizi kodi itasaidia wakulima wetu wapate bei nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, naomba nizungumzie Taasisi ya TSC (Teachers Service Commission). Niishukuru Serikali kwa kuanzisha hiki chombo ambacho kimelenga kutetea maslahi ya walimu nchini, lakini toka mwaka jana baada ya kuunda sheria sijaoana mchakato ambao unaonesha kwamba kweli hiki chombo kimejipanga kutatua kero za walimu nchini. Sijasikia katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ikizungumzia wamejipanga vipi katika rasilimali watu na fedha kuhakikisha TSC ina take off, na ukiangalia changamoto za walimu bado zipo, arrears za walimu bado hazijalipwa asilimia 100. Na nikizungumzia Karagwe naamini changamoto hii pia ipo katika nchi nzima, suala la kupandishwa madaraja walimu lakini effect ya payment inachelewa. Sasa TSC ingekuwa imeshaanza naamini sasa hivi wangekuwa wako katika kutatua hizi changamoto, kwa hiyo nipende kuiomba Serikali, TSC ni chombo muhimu cha kutetea maslahi ya walimu nchini, kipeni rasilimali watu na fedha ili kiweze kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la wigo wa kodi. Ukiangalia historia ya uandaaji wa bajeti za Serikali, kwa kweli bado tuna narrow tax base, ifike mahali Wizara ya Fedha na Mipango na Serikali kwa ujumla muangalie avenues nyingine za kodi ili tuweze ku-broaden tax base. Wale existing tax payer’s itafika mahali watakuwa wanakuwa disincentivized kuendelea kulipa kodi kwa sababu kila mwaka tunaongeza increments kwenye tax items hizohizo, tunashindwa kuwa wabunifu wa vyanzo vipya vya mapato ili tax base ipande, mapato yakue bila kuweka burden kubwa kwa wale honest tax payers na katika hili niiombe Serikali muandae mkakati wa kuleta informal sector kwenye formal sector ili huu mkakati wa ku-broaden tax base uendane na kuingiza informal sector kwenye formal sector ili tuweze kukuza mapato nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nizungumzie suala la Dar es Salaam Stock Exchange. Serikali yetu kwa muda mrefu imekuwa ikijitahidi kuweka sera za kukuza Dar es Salaam Stock Exchange, lakini nimeshangaa katika bajeti hii ambayo imewasilishwa tunapiga hatua tatu mbele, halafu tunakwenda hatua nne nyuma. Capital gains tax on sales of shares, kwa kweli Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, nikuombe sana, kwa kufanya hivi tutakuwa tunaua Dar es Salaam Stock Exchange isiweze kushindana na stock exchange nyingine ambazo ziko Afrika Mashariki, na ni mkakati mmoja wapo wa kuisaidia nchi yetu tuweze kupata mitaji ya kuwekeza kwenye uchumi wetu wa viwanda kupitia kwenye Dar es Salaam Stock Exchange. Na hii ni dalili ya kuwa na narrow tax base ambayo inaangalia low hanging fruits, twende kwenye high hanging fruits, najua ni kazi lakini naamini kwa uwezo wako mahiri na Wizara yako kwa kushirikiana na Wizara nyingine mnaweza, hii kodi ya capital gain tax on sales of shares naomba muiondoe Mheshimiwa Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la mwsiho. Karagwe, NSSF ilikuwa na lengo zuri la kushirikiana na Vyama vya Ushirika kutoa mikopo ya bei nafuu kwa wananchi lakini ule mchakato ulikwenda ndivyo sivyo. Kuna wananchi wengi Jimbo la Karagwe walitozwa hela, wengine mpaka kufikia shilingi 280,000 kwamba watapata mkopo wa bei nafuu na baadaye wataingizwa kwenye Bima ya Taifa. Huu ni mpango mzuri, niombe Serikali i-review huu mkakati lakini pia izungumze hizi fedha ambazo wananchi wangu walitoa kwa ajili ya kupata mikopo ya bei nafuu na Bima ya Taifa wanarudishiwa lini na kama hawarudishiwi basi turudi kwenye huu mpango, uwe reformed uweze kuwasaidia wananchi wa Karagwe na nchi nzima kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja, ahsante.