Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MWANNE I. NCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Balozi, Dkt. Augustine Philip Mahiga, Naibu Waziri Dkt. Susan Kolimba na Katibu Mkuu wa Wizara kwa hotuba nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara yetu iangalie sana mipaka yetu ambayo ina vichocheo vingi na ambavyo wahamiaji haramu hupenya hasa kwenye mipaka ya Kenya na Tanzania kwa kupitia njia za Arusha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu masoko ya ujirani mwema; elimu itolewe. Hapa nchini kuna wafanyabiashara wadogo ambao wanasafirisha bidhaa zao kama mahindi, mpunga, kahawa, chai ili wafanye biashara kwa weledi, kwani mikoani hakuna elimu ya kutosha. Waheshimiwa wetu ambao ni Wabunge wa Afrika Mashariki wapewe uwezo wa kuzunguka nchi nzima kutoa elimu hata mashuleni na vyuoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la utumishi; Wizara hii iwasiliane na Wizara ya Mambo ya Ndani kuongeza Watumishi wa Uhamiaji ili ajira iongezeke na kusaidia kulinda mipaka yetu kwani mpaka sasa bado watumishi hao ni wachache. Pia suala la utalii Waheshimiwa Mabalozi watangaze vivutio vyetu vilivyopo nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.