Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na pongezi kwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara kwa kuwasilisha hotuba yao hapa Bungeni ili tuweze kuijadili. Yapo mambo ambayo naomba kupatiwa ufafanuzi na mengine napenda kuishauri Serikali yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kubadilishana wafungwa wa Tanzania na nchi nyingine. Naomba ufafanuzi wa kama upo uwezekano wa Watanzania ambao wamekwenda nchi nyingine wakapata makosa ya kuhukumiwa kifungo, je kuna uwezekano wa wafungwa hao kurudishwa kuja kufungwa hapa nchini au kama kuna uwezekano wa kubadilishana na wafungwa walio hapa nchini kwenda kufungwa katika nchi zao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo napenda kujua kama Watanzania waliopo nje ya nchi wakikutwa na makosa, Serikali inawapa msaada wa kisheria, kwa vile najua wengine wanafungwa kwa sababu hawana uwezo wa kuweka Mawakili wa kuwatetea, kama nchi ni msaada gani unatolewa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, vifo vya Watanzania waishio nje ya nchi; hivi karibuni yamejitokeza matukio ya mauaji ya kutisha baadhi ya vijana wa Kitanzania wanaoishi nchi za nje kama USA kuuawa kwa kupigwa risasi; je, ni jitihada gani ambayo Serikali yetu inachukua kubaini hayo? Ningependa kujua jitihada za Serikali kuhusiana na hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali kuwaunganisha wajasiriamali wa Tanzania kuingia ubia na makampuni ya China. Serikali ya Awamu ya Tano, sera yake kubwa kufufua na kujenga viwanda kwa ajili ya kujenga uchumi wa nchi na kuongeza ajira. Kwa kuwa nchi ya China katika hilo ipo mbali sana ina viwanda vidogo vidogo na vikubwa, napenda kujua Tanzania imejipanga vipi kuhakikisha inaingia ubia na makampuni ya China yatakayoweza kusaidia ukuaji wa viwanda vyetu nchini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata bahati ya kutembelea Ubalozi wa Tanzania nchini China na UK, kwa kweli jengo la Ubalozi wa Tanzania China lilikuwa na hali mbaya sana. Je, ni utaratibu gani huwa unatumika katika kupeleka pesa za ukarabati wa majengo hayo kwa sababu ni aibu sana Mabalozi wetu kuishi katika mazingira mabaya na magumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.