Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami nichangie Wizara hii ya Mambo ya Nje kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua Serikali inawatumiaje Mabalozi waliopo nje ya nchi katika kutangaza nchi yetu kwa maana ya ushiriki katika majukwaa ya kiuchumi. Mfano sekta ya utalii inachangia pato la Taifa kutokana na fedha za kigeni takribani asilimia 25. Mheshimiwa Waziri atakapohitimisha naomba aniambie wana mpango gani wa kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza Tanzania ili kuendana na kasi ya kukua kwa uchumi wa kati na uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto kubwa ya Mabalozi hawajui vizuri nchi na vivutio vilivyopo. Ofisi za Mabalozi hazina wataalam wa utalii ambao wanaweza kuitangaza nchi yetu kupitia Balozi zetu. Naomba Mheshimiwa Waziri anipe majibu wana mpango gani kuwa na Maafisa wa Utalii katika Balozi zetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kufahamu ni namna gani wanafunzi wanaosoma nje ya nchi wanapata misaada kupitia Balozi zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.