Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa na kuaminiwa na wananchi wa Tanzania kuwa Rais wa Awamu ya Tano. Nampongeza pia Mheshimiwa Rais kwa kuunda Baraza la Mawaziri lenye ueledi wa hali ya juu wakiwemo Waziri na Naibu Waziri wa Wizara hii ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache ya kuishauri Serikali kupitia Wizara hii likiwemo suala zima la mabalozi wa utalii. Tanzania ni nchi ambayo imejaliwa kuwa na vivutio vya aina mbalimbali na vingi. Naishauri Serikali iwahimize Mabalozi wetu walio kwenye nchi mbalimbali watangaze utalii na vivutio vyetu ili nchi yetu ipate watalii wengi, iwe ni miongoni mwa kazi na wajibu wa Balozi kutangaza vivutio na utalii wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee ama nishauri kuhusu ulinzi wa Watanzania wanaoishi ughaibuni. Serikali ichukue hatua za makusudi kuhakikisha wananchi ama Watanzania hawa wanaoishi ughaibuni maisha yao yanakuwa salama kwa maana ya uhai. Matukio mengi ya kikatili yameendelea kuripotiwa wanayofanyiwa Watanzania hawa ikiwemo mauaji na vitendo vya udhalilishaji. Serikali ijitahidi kupunguza ama kuondoa kabisa kupitia Balozi zetu vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa Watanzania hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri mwenye dhamana amezungumzia ukarabati wa majengo ya Balozi zetu. Nami naomba nitumie fursa hii kuishauri ama kuomba Serikali ihakikishe inaipatia Wizara hii fedha ya ukarabati wa majengo ya Balozi zetu kama ilivyoombwa na kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.