Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HAFIDH ALI TAHIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nichukue fursa hii kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ndogo ya kutoa mchango mdogo nilionao katika Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka Wizara ifahamu kwamba Wizara hii kwa nchi za nje ndiyo jicho la Tanzania. Tunapotaka Balozi zetu zifanye vizuri basi Tanzania ndipo itakapoweza kujitosheleza katika kuonesha kwamba na wao wamo katika sura ya ulimwengu. Hata hivyo, kama Wizara hii haikufanya bidii katika kuhamasisha na kuziweka Balozi zetu vizuri kazi tunayoifanya itakuwa bure.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeanza na hilo kwa sababu kuna matatizo mengi ambayo yanazikabili Balozi zetu hivi sasa ukiachilia mambo ya utendaji, lakini kuna tatizo sugu la wafanyakazi wanaostaafu kutorudishwa nyumbani, hawapewi marupurupu yao lakini wafanyakazi wengine wanatoa sababu ambazo hazina msingi kwa kusingizia wana watoto wanasomesha walipofanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ichukue hatua, kama wanaweza kuwastaafisha wafanyakazi wawastaafishe, wawalipe haki zao na warudishwe nyumbani. Kama hawawezi wasiwastaafishe na kutoa tamko rasmi kwamba wafanyakazi hao bado ni wafanyakazi katika Balozi zetu. Hili ni tatizo kubwa katika Balozi zetu na lazima Wizara ichukue hatua kuhusiana na wafanyakazi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili limezungumzwa sana hapa nalo ni suala la majengo. Majengo ya Balozi za Tanzania ni aibu. Usije ukajaribu kwenda Maputo au Zambia utaona aibu sana. Kwa nini tunachuka hatua za kutokuwapa pesa Mabalozi wetu katika Balozi mbalimbali lakini wakati huo huo Wizara hii utasikia wanataka kuongeza Balozi nyingine katika nchi za nje. Tuhuishe hizi zilizokuwepo halafu tutafute nyingine, tusijitangaze tunataka kufungua Balozi nyingine wakati tulizokuwa nazo hatuwezi kuzihudumia. Hili ni tatizo kubwa ambalo linawapeleka wafanyakazi katika Balozi zetu kuonekana kwamba labda wao ni ombaomba na kama hawawezi kutoka Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine namwomba sana Mheshimiwa Waziri wakati umefika hivi sasa Balozi zetu kupewa nafasi ili ziweze kujitetea katika bajeti zao. Bajeti zinazopelekwa kule ni finyu kutokana na kazi ambazo wanafanya kwa sababu hakuna mtu ambaye anashirikishwa katika kutetea bajeti za Balozi zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tarehe 22 Aprili, katika Bunge lako hili nilikuwa nimezungumzia suala linalotia aibu Tanzania na linalotia aibu Balozi zetu nje ya nchi. Wakati nilipokuwa nauliza swali hilo Mheshimiwa Naibu Waziri alijibu kwa kufyatua tu jambo ambalo mimi halikuniridhisha na mpango wa kufyatuliana majawabu katika Bunge hili unakuwa haupendezi. Tunapouliza mambo ya msingi tujibiwe kimsingi na ukweli ulivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nazungumzia deni la Tanzania katika hospitali moja kule London inayoitwa London Bridge ambapo kuna pound 79,000 zinazodaiwa Tanzania na narudia tena inadaiwa Tanzania. Kilichojitokeza hapa kuna Mtanzania mmoja anatokea Zanzibar alifanyiwa matibabu London kaenda bila kujulikana na mtu yeyote lakini Ubalozi ulichukua hatua ya kumpa matibabu Mtanzania yule. Hospitali imepeleka barua ya gharama katika Ubalozi wetu London na Ubalozi umepeleka barua katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.