Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa ya kuchangia katika Wizara ya Mambo ya Nje. Kwa utangulizi tu, nianze kwa kuonesha masikitiko yangu juu ya ukandamizwaji wa demokrasia unaofanywa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hili Bunge sasa limegeuka kuwa mwiba mkali sana kwa ustawi wa demokrasia ya nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono jitihada zote zilizofanyika siku ya jana kuhakikisha kwamba tunaleta attention ya kuwasaidia vijana wetu ambao hawakutendewa sawa. Whether mliikubali au mliikataa lakini ulimwengu unajua ya kwamba hapo mmekosea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mheshimiwa Msigwa umefanya kazi yako vizuri, hongera sana. Naomba pia kuunga mkono hotuba ya Kamati ya Mambo ya Nje, mmefanya kazi nzuri, mmetendea haki mlichokiona na huo ndiyo ukweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ku-declare kwamba ni mjumbe wa Kamati hii na katika kutekeleza majukumu yetu ya Kamati, nieleze tu masikitiko yangu kwamba hii ndiyo Wizara ambayo tulikuta hata cha kuzungumzia hakipo, kila unakogusa tabu, shida, karaha, fadhaha. Ukizungumzia shughuli za utendaji wa watendaji katika Wizara ya Mambo ya Nje yaliyoko kule fadhaha, ukitazama Balozi zetu zilizoko nchi za nje fadhaha, bajeti ya maendeleo waliyotengewa hawakupata hata senti moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikitika kwa kweli kuona hotuba hii ambayo nimeisoma mwanzo mwisho, sijajua Waziri anaogopa, ana hofu au ana mashaka, lakini nilitarajia aje na hotuba ambayo ni ya kitaalam, ina mikakati na ina mipango lakini Mheshimiwa Waziri amekuja na hotuba ya kisiasa. Nikajiuliza yale tuliyoyaona wakati wa Kamati, japo sawa Waziri mpya kwa this time, nikajua atayaona na kwenye hotuba yake ndiko atakakokuja na yale ambayo aliyaona ni upungufu na ataonesha mikakati yake na way forward lakini Mheshimiwa Waziri ameandika siasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kwenye hotuba yake ukurasa wa 111, amesema malengo ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2016/2017, nimeyasoma yote ni siasa. Nisome mawili ya mwanzo tu, la kwanza kutangaza nchi yetu kama moja ya nchi duniani zenye mazingira mazuri kwa ajili ya uwekezaji kutokana na historia yake ya miaka mingi ya amani, umoja, utulivu na mshikamano wa kitaifa, kwa kufanyaje?
Lla pili, anasema kuongeza uwakilishi wetu nchi za nje kwa kufungua Balozi mpya ofisi za Kikonseli na kuimarisha rasilimali watu na fedha wakati haya ndiyo ambayo kwenye Kamati tumezunguka tukiyatazama, hizo Balozi tulizonazo tu ziko hohehahe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia Mheshimiwa Mbunge, mama wa CUF anasema alikwenda Msumbiji akakuta katika Ofisi ya Balozi mama ntilie anaingia anauza chai, hakuna hadhi. Mimi iko Balozi tulifika tukakutana na mende, panya na popo. Sasa akituambia tu kwa maneno mepesi kama alivyosema katika lengo lake la pili kwamba anataka kufungua Ofisi za Balozi wakati viwanja tulivyonunua havijajengwa, viwanja vilivyotolewa havijajengwa, nyumba tulizopewa kwa ajili ya Ubalozi ziko hoi, ndiyo hizo zenye popo na mende, sasa anafunguaje Balozi nyingine mpya wakati zilizopo hii ndiyo hali yake? Basi fine, tulitegemea aseme at least kwa details kwamba tutafanya moja, mbili, tatu, tutakarabati lakini tutaongeza na hili yaani tulitaka hata kuona nyingi ngapi? Ndiyo maana nasema hii ni siasa kwamba tutafungua Balozi mpya, ngapi, wapi na kwa gharama ipi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni huduma za kibalozi. Watendaji wetu katika Balozi zetu mbalimbali wana hali mbaya, huduma ni shida lakini hata vipindi vyao vya kuhudumia vinapokwisha fedha ya kuwarejesha nyumbani ni tatizo. Badala yake, kama alivyosema Mheshimiwa Msigwa, uteuzi wa nafasi za Balozi katika nyakati fulani zimeonekana ni adhabu kwa wale watu ambao wanaonekana ni threat kwa wanasiasa fulani. Kilicho kibaya ni kwamba unapigwa jina Ubalozi halafu unaachwa hapo. Kwa hiyo, pale Foreign Affairs kuna watu wenye titles za Ubalozi wengi tu, wakiona unakerakera kwa kuweko hapa basi wanakutafutia mahali wanakwenda kukuficha pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri atakaporejea ningetamani haya ninayoyazungumzia atuoneshe kimkakati hasa kwamba anakwenda kuchukua hatua gani na atupe na time frame. Kwa sababu hata suala la Sera ya Mambo ya Nje, hii ambayo imetumikiwa kwa miaka kadhaa sasa ya Economic Diplomacy, hakuna tulicho-achieve. Kwa sababu kingekuwepo angekuja nacho akatuonesha kwamba kwa kipindi kilichopita tumefanya yafuatayo lakini hotuba yake imeongea siasa mwanzo mwisho na hakuna ambacho kiukweli amemudu kutupatia kama takwimu za kuonyesha achievement na if so, what is next? Je, tunakuja na sera nyingine au bado tunaendelea kutumikia hiyohiyo iliyoshindwa? Mchangiaji mmoja amesema tumeleta wawekezaji wa kutosha. Sawa, walipotosha wakafanya nini? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la utangazaji wa vivutio na fursa za uwekezaji Tanzania, kama alivyosema Mheshimiwa Mwanjelwa, natamani sana labda tungeweka sasa goals na kila Afisa wa Balozi aliyeko Ubalozini ambaye ana wajibu wa kutekeleza haya mwisho wa bajeti ya mwaka mmoja atuambie ame-achieve nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua hawauwezi kumdai ame-achieve nini kwa sababu hawawa-finance, hawawa-facilitate wale watu, kwa hiyo hawa-perform. Wamekaa kule wanaendelea ku-enjoy diplomatic securities lakini kiukweli najua hawawezi kukubali ku-set goals na kuanza kufanya assessment ya performance kwa sababu hawajawa-facilitate maafisa wetu walioko maeneo ya Balozi ili waweze kutekeleza wajibu wao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niiombe Serikali itusaidie katika Wizara ya Mambo ya Nje, bajeti wanayopewa haikidhi haja hasa kwenye miradi ya maendeleo. Ile ndiyo sura ya Tanzania katika maeneo ambayo tuna uwakilishi lakini kama kweli tuna Balozi ambazo mapaa yanavuja na umekaa sitting room mende anapita, kiukweli hata kama tungetaka wafanye nini isingewezekana kwa sura ile. Mwaka jana wametengewa bajeti ya shilingi bilioni nane lakini hawakupata hata senti moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Diplomasia. Kama kweli majukumu tuliyokipatia Chuo cha Diplomasia ndiyo tunayotaka kitekeleze, basi Serikali inatakiwa kuja na kauli ituambie kwamba hicho chuo kweli ni Chuo cha Diplomasia au wameshabadilisha ajenda. Kile chuo kwa miaka mitatu mfululizo hawajapata senti moja ya pesa za maendeleo halafu tunasema wawafundishe Mabalozi wetu, wake wa Marais na kadhalika, hiyo haiwezekani unless tuwe na mkakati mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.