Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, unapokuta maji yakoge, mwanzo hujui mbele kama utayakuta tena.
Kwanza nichukue fursa hii kukushukuru wewe kunipa hizi dakika nne au tano hizi zilizobaki kumalizia ngwe hii iliyobaki na nitakuwa si mwingi wa fadhila kama sikumshukuru Mwenyezi Mungu, aliyeniwezesha kusimama hapa na kuvuta pumzi zake na kurudi tena kwa mara ya pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo Mheshimiwa Waziri kipindi kilichopita mwaka jana, nilikigusia sana na nikazuia shilingi, na hii leo hii nafikiri Mheshimiwa Waziri kuna vijana 13 kutoka Zanzibar. Nazungumza kuhusu maslahi ya Zanzibar kuhusu Wizara hii, kutokana na mambo yanayohusu masuala ya Muungano.
Kuna vijana 13 mmewasomesha Chuo cha Diplomasia, bahati mbaya mkawachukua saba, lakini kwa masikitiko makubwa na unyonge na huruma kubwa mpaka hii leo vijana hao saba hamjawaajiri. Mwaka jana nilihoji kwenye bajeti na Mwenyezi Mungu si Athumani kanirudisha tena leo hii, nipo hapa, kwa hiyo, nitahitaji maelezo ya vijana saba hawa wa Zanzibar mpaka leo hamjawaajiri na hii ilikuwa si hisani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni makubaliano katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Vijana hawa hamjawaajiri hadi hivi leo, nataka maelezo ya kina kuhusu suala hili na umri wao unakwenda, na mmechukua barua Zanzibar kama kuwaazima, si kitu kizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, natoka hapo kwa haraka haraka nitahitaji maelezo lakini haya vilevile ni ya kusikitisha, Wizara hii huko nyuma au uzoefu unaonesha Waziri anatoka Bara, Naibu Waziri kutoka Visiwani. Lakini kwa masikitiko Wizara hii wote wazee mmekalia kiti chenu, lakini si maamuzi yangu ni maamuzi ya Mheshimiwa Rais. Lakini kama hapatoshi hapo, hata Wizara ya Fedha haya mambo ya Muungano tulikuwa tupokezane, hapatoshi hapo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumshukuru Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kwa umakini wake na Mwenyezi Mungu ampe umri mrefu, alikuwa akijitahidi katika safari za nje, kuwachukua Mawaziri kutoka Zanzibar katika safari zake, je, mpango huu utaendelea tena vilevile au utalala?
Mheshimiwa Mwenyikiti, nitoke hapo nataka kuulizia haya maslahi ya Mabalozi wangapi wa Zanzibar waioajiriwa, huu ni wimbo wa Taifa wa muda mrefu. Wimbo huu umekuwa wa muda mrefu, kuhusu ajira katika Wizara hii nataka kujua Mabalozi kutoka Zanzibar ni wangapi wanaowakilisha hivyo? Vilevile senior officer kutoka Zanzibar, katika Mabalozi wako wangapi, wimbo huu umekuwa ni wa muda mrefu lakini hautoshi...
MWENYEKITI: Ahsante,