Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata nafasi hii, kuna mengine sikupanga kuyasema lakini kutokana na maelezo ya Waziri Kivuli, nimejikuta kwamba nawajibika kuyasema. Sisi wengine background zetu zinatuongoza kusema hivi ambavyo nitasema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme moja tu kwamba tujifunze kua-appreciate, the way Waziri Kivuli amewasema Mabalozi, kwa kweli kwanza kitendo cha kuwafananisha na Mabalozi wa Nyumba Kumi, maana yake ni kwamba ni kama vile Mabalozi wa Nyumba Kumi wao sio watu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ninaamini Mheshimiwa Msigwa, ili atambulike popote lazima aende kwa Balozi wa Nyumba Kumi. Lakini pia Mabalozi hawa wameisha fanyakazi nzuri ya kuwakilisha Taifa letu, hii ni nchi ambayo hakuna kiongozi mkubwa duniani hajafika katika nchi hii, haya ni matokeo ya kazi nzuri ya hawa Mabalozi. Clinton ameisha fika hapa, Obama katika utawala wake mpaka sasa hivi amefanya jumla ya ziara 46, katika nchi zaidi ya 150 duniani, katika hizo 46 amefika hapa, ni kutokana na kazi nzuri ya hawa Mabalozi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Marais wa nchi kubwa kama China, Hu Jintao ameondoka alikuja hapa, ni kazi nzuri ya hawa hata huyu wa sasa. Sasa ndio maana nasema tujifunze ku-appreciate na kutiana moyo kuliko kusemana semana kwa namna ambayo haitusaidii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niseme tu kama alivyosema Mheshimiwa Lusinde, yaani kweli kuna time ya kupinga lakini sio kupinga tu. Mheshimiwa Dkt. Jakaya alikuwa anasafiri anapingwa, huyu sasa hivi hasafiri ameamua kutanua wigo kwa Mabalozi unapinga, where are you standing you guys? Anyway niendelee kujilinda na background yangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite sasa kwenye Sera ya Mambo ya Nje, hii economic diplomacy. Nimshauri Mheshimiwa Waziri na Wizara kwa ujumla, hebu tujaribu kuona je, sera hii inaendana na current situation? Wakati sera hii inapoanzishwa mwaka wa 2001, je, changamoto kwa mfano kama mambo ya global warming, mambo kama ya vikundi vya kigaidi, mambo ya kuibuka kwa jumuiya nyingine mpya za kiuchumi, kama the BRICS yalikuwepo, na kama hayakuwepo sera imejipanga vipi, au Wizara imejipanga vipi ku-accommodate hali kama hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ningeshauri Wizara iwe na kitengo au na idara maalum ambayo kazi yake itakuwa ni kusimamia utekelezaji na kufanya tathmini ya diplomasia ya kiuchumi. Nijikite katika suala la EAC, ni kweli kwamba katika siasa za kimataifa za sasa hivi you can‟t work alone, lazima uwe katika economic integration, katika economic blocks. Lakini pia na sisi kwenye hizi blocks tujitizame, hebu tuangalie pia ni namna gani tunaweza ku-benefit nje ya EAC. Nitatoa mfano kwa mfano, DRC trade wise mizigo ambayo tunasafirisha kwenda DRC volume wise inazidi ya Rwanda, Burundi na Uganda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hata kama tutajenga reli, tutaimarisha bandari, kama hatutailinda DRC, strategically kama huyu ni partner wetu kibiashara, kwa sababu ya kwenda na mkumbo wa Single Custom Territory nawaambia tutapoteza na ili tufanikiwe na kulinda soko la DRC kibiashara, lazima Lubumbashi tufungue ubalozi mdogo, hili halikwepeki, kusudi tulinde maslahi ya Kongo.
Lakini pia sisi tunashiriki Congo Peace Keeping na kadhalika, we are not going there kama shopping hapana, nchi zote duniani Amerika unaona wanaenda Iraq, na kadhalika baada ya pale ni kuulinda na kung‟amua fursa za kibiashara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, fursa zilizoko Kongo, hebu tujaribu kuzilinda. Lakini pia Mheshimiwa Waziri hata hii Single Custom Territory, leo hii nasikia kwamba tumekubaliana na wenzetu kwamba after sometimes tutapiga marufuku mitumba. Je, ndani hapa viwanda vya nguo tumejipanga sisi, au tutakuwa soko la wa Kenya, kama ambavyo leo hii maziwa ukienda kwenye maduka yanatoka Kenya, ukienda walimu katika kila shule tano, tatu unakuta ni walimu kutoka nje. Sawa tunaonesha spirit ya EAC lakini pia na sisi kama hii Wizara ya ku-coordinate mambo kama hayo, tunajipanga vipi, Mheshimiwa Waziri ningependa katika kujumuisha, uje na masuala kama hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine la muhimu JPC. JPC zetu kwa kweli zimekuwa tu za kinadhalia. JPC ni muhimu katika kutatua changamoto na kuchochea uhusiano hasa uhusiano wa kiuchumi. Hebu tutenge fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunafanya hizi JPC (Joint Permanent Commission) maana yake ndio mwanzo na chemchem ya mahusiano. Lakini hayo yote Mheshimiwa Waziri utakapoyajumuisha, ili haya yote tuweze kuyafanikisha vizuri lazima tuangalie staff welfare. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanadhani wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje wanalipwa mishahara in terms of dollar, Kumbe maskini ya Mungu wanalipwa ni terms of TGS shillings. Lakini sio hivyo tu hata Balozi zetu Mheshimiwa Rais katika kubana matumizi, amesema kwamba kazi nyingi zitafanywa na Balozi zetu, tumezi-equip kwa kiasi gani na tunazi-facilitate kwa kiasi gani? Je, zina staff wa kutosha? Sio mtumishi yuko nje ughaibuni, lakini nyumba kila mwisho wa mwezi unapofika, roho yake iko juu kwamba mwenye nyumba atakuja kudai pango, unategemea huyu mtu ata-deriver? Unategemea huyu mtu ata-perform? Maendeleo ni gharama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuje na mipango ambayo pia itaangalia staff welfare. Hata pale Makao Makuu Wizara ya Mambo ya Nje, mimi nimetoka pale nafahamu, watu wanafanya kazi usiku na mchana, Mheshimiwa Waziri hili unalifahamu, kwa hiyo tuangalie ni kwa namna gani tutaenda, lakini pia katika diplomacy ili uwe a good diplomatic person, lazima pia u-save abroad. Sasa huwezi kuwa a good diplomat unakaa headquarter miaka kumi, kumi na tano. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie pia suala la posting, kwa sababu kama tunakusudia watu hawa wafanye kazi ipasavyo lazima tuwa-expose. Lazima tuangalie welfare yao, lazima tuwatafutie short training za mambo ya diplomasia ya kiuchumi ili kweli tuendane na kasi ya mambo ya dunia ya sasa inavyokwenda. Namshukuru Mheshimiwa Rais, amempa Wizara mtu ambaye ni nguli wa mambo haya, huyu mtu ameongoza ushauri katika mgogoro wa Somalia mpaka leo hii Somalia ina Serikali, jambo ambalo hata wa Marekani walishindwa. Leo hii mnawasema eti Mabalozi hawafanyi kazi, maana yake huyu katoka katika kitu cha aina hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nikuombe utakapokuwa unajumuisha, tafadhali ili tuenende sambamba na demokrasia ya kiuchumi, tuzingatie kufufua JPC kivitendo sio kwa maneno. Lakini tuangalie welfare ya watumishi katika Balozi zetu, lakini pia na watumishi pale headquarter, lakini kuhakikisha pia watumishi wanakwenda posting.
Napenda kuishukuru Wizara, Katibu Mkuu, Wakurugenzi wote, kwa kazi inayofanyika nzuri na tunaendelea kuwatia moyo, msikatishwe tamaa na maneno ya kukatisha tamaa. Sisi tusonge mbele Mungu awabariki sana.