Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, nisamehe. Ni mdogo wangu, Mheshimiwa Dokta Ashatu Kijaji, Mbunge wa Kondoa Vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yoyote haiwezi kuendelea bila kulipa kodi, kodi ndiyo msingi wa maendeleo. Kwa hiyo, kila mwananchi anatakiwa kulipa kodi kabla hajadai huduma lakini Watanzania tumezoea kudai huduma bila kulipa kodi. Tunadai hospitali, barabara, maji, umeme lakini ni wangapi wanaolipa kodi kwa uhakika? Wafanyakazi ni walipa kodi kwa uhakika kwa sababu pesa zao hawazikamati mkononi, wanakatwa kodi moja kwa moja. Ifike wakati sasa wananchi wa Tanzania tufurahie kulipa kodi ili maendeleo tunayoyataka tuyapate kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, sipingani na azma ya Serikali ya kuanzisha viwanda lakini tunapofikiria kuwa na viwanda tufikirie pia kuwa na malighafi. Tunasema mazao yanaoza; mazao gani yanayooza? Tunasema matunda yanaoza Muheza, Ukerewe na maeneo mengi lakini je matunda haya yapo mwaka mzima kiasi kwamba tukiwa na viwanda vitano vya kukamua juice watapata malighafi ya kutosha? Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha mashamba makubwa kwa ajili ya malighafi kwa viwanda tunavyovipigia kelele? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lazima Serikali iweke mkakati madhubuti wa kuwa na mashamba makubwa ambayo pia yatazalisha ajira. Kwa hiyo, tuwe na mashamba makubwa tukilenga viwanda ambavyo tunataka kuvianzisha lakini tukisema tunaanzisha viwanda ku-create ajira bila malighafi viwanda hivyo haviwezi kufanya kazi. Kwa hiyo, tulitazame suala hili kwa upana wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwa mkulima ni nani anayejali mkulima huyu kalima nini? Je, katumia mbolea? Je, analimaje? Je, anatumia zana gani? Maafisa Ugani wetu hakuna anayejali na hawatoshi hasa katika maeneo yetu ya vijiji. Kwa hiyo, kuna haja Maafisa Ugani kuwaweka wakulima katika hali ya kujua kwamba sasa malighafi kwa ajili ya viwanda vyetu inatakiwa na wawaelekeze wakulima kulima kwa lengo la kupata mapato zaidi kwa ajili ya kuendeleza viwanda vyetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna suala la kupata mapato, tumesema tunataka kodi ili tuwe na fedha za maendeleo kwa ajili ya Taifa letu. Hata hivyo, kuna suala la ubia kwa maana ya Serikali kuingia ubia na mashirika mbalimbali na watu binafsi lakini utekelezaji wa suala hili ni mdogo sana. Suala la ubia tumeliongea kwa muda mrefu sana katika Bunge hili lakini ni makampuni mangapi yameingia ubia na Serikali? Je, ni mashirika mangapi yameingia ubia na Serikali?
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe mfano mdogo tu, sisi tulipelekwa Malaysia mwaka 2008 ili Wamalay waje wajenge barabara ya Chalinze – Dar es Salaam wakishirikiana na NSSF mpaka leo hatujaambiwa tatizo ni nini? Tungepata pesa kwa sababu wale wange-charge kodi kidogo kwa ajili ya kuendesha ile barabara lakini mpaka leo suala la ubia linakwenda taratibu mno katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, NSSF walikubaliana na watu wa Malaysia kwamba watajenga magorofa 25 Ilala Mchikichini mpaka leo hakuna kinachoendelea. Hatuwezi kusema tunataka maendeleo, tunataka ubia wakati utekelezaji wa suala la ubia linaenda taratibu mno tatizo ni nini? Lazima tujue tatizo liko wapi? Hata tunaposema tunafufua viwanda, hawa watu wa viwanda wameulizwa mnakumbana na matatizo gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tujiulize walikumbana na vikwazo gani na tumeandaa akili zetu kupambana na changamoto tutakazokutana nazo katika masuala ya viwanda? Hili suala la PPP ni muhimu lazima kuliangalia. Tuwaulize NSSF kilichokwamisha ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam – Chalinze ni nini? Watuambie kilichokwamisha ujenzi wa nyumba zile ni nini? Tungepata mapato mengi kutokana na suala hili, naomba tuliangalie.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna haja ya kuangalia mashirika yasiyo na tija. Ngoja niwape mfano, tangu tuanzishe RUBADA wamesha-deliver nini kwa Serikali hii? Kuna watu waliomwambia Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwamba RUBADA tu inaweza kulisha Taifa hili lakini RUBADA iko wapi? Mpaka leo RUBADA wanapewa ruzuku. Mashirika yasiyo na tija yaondoke sasa kama kweli tunataka kupata maendeleo. Hakuna haja ya kuwapa ruzuku, wanalipwa mshahara, wanalipwa per diem za safari lakini hakuna tija, hili ni vizuri tukaliangalia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna tatizo kubwa la fedha Tanzania shillings kutotumika katika mauzo au manunuzi, tatizo ni nini? Suala hili tumelisema mpaka tumechoka. Naomba Waziri wa Fedha hebu suala hili lifanyiwe kazi sasa, nchi nyingi zilizoendelea wanathamini pesa zao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tozo kwa watalii limeongelewa sana. Wabunge tujiulize kuna makampuni yalirudisha vitalu 13, kwa nini vilirudishwa? Lazima tujiulize kwa nini vilirudishwa ili tujue tanaanzia wapi kuliko kuanza na tozo wakati wenzetu Kenya wameondoa tozo.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme lingine, tumechoka sisi wa Dodoma kila siku tunaambiwa Makao Makuu ya Serikali ni Dodoma lakini hatuoni kinachoendelea. Mashirika ya Umma, Ofisi za Serikali, mnajenga majengo Dar es Salaam, hivi mna dhamira ya dhati ya kuhamia Dodoma? Mimi nilileta Hoja Binafsi ili mtuambie kwa nini hamtaki kuhamia Dodoma? Mnatupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, hatutaki! Mtuambie kwa nini hamtaki kuhamia Dodoma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma hana hata ofisi, Manispaa tutakwenda kumfukuza pale alipo ili mumtafutie pa kufanyia kazi zake. Hamtaki kuhamia Dodoma na hamtaki kumjengea Mkuu wa Mkoa ofisi yake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Mkungunero linatuumiza, Serikali hamtaki kulizungumza kwa nini? Wananchi waliomba heka chache sana kwa ajili ya kilimo, Maaskari wale wa Wanyamapori hawapiti kwa wananchi, hawapiti pale barabarani kwa sababu kuna uhasama mkubwa na Serikali haitaki kulishughulikia. Ninawasihi hebu suala la Mkungunero lifike mwisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, wanawake wa Mkoa wa Dodoma hawajatua ndoo vichwani na mvua inanyesha miezi miwili tu hapa Dodoma. Ukisema suala la maji, Waziri wa Maji anaturemba tu hatuelewi anachotusaidia. Tunaomba sasa, kama kweli Serikali ina dhamira ya kuhamia Dodoma tuanze kuwasaidia wananchi wa Dodoma, tumtue mwanamke wa Dodoma ndoo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wanawake wanaamka saa tisa, ndiyo maana wanaume wa Dodoma wengine wameoa wanawake wanne, anafanyaje? Yeye ni Mkristo kila siku saa tisa mwanamke yuko barabarani kwenye maji, hatuwezi, jamani mtufikirie katika hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Dodoma kuna Wilaya zilizoanza; tuna Wilaya ya Chemba, Wilaya ya Bahi ilianza siku nyingi hakuna maji, hakuna umeme, Mheshimiwa Badwel ameomba mpaka amechoka, Mheshimiwa Nkamia ameomba mpaka amechoka, tatizo ni nini kwa Wilaya za Dodoma? Bahi pale maji ni ya chumvi, huwezi kuoga, huwezi kunywa hata mnyama hanywi, kila mwaka tunaomba maji Dodoma, tatizo ni nini?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini msisahau kumuongezea CAG…