Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai na kufika hapa katika Bunge lako hili Tukufu. Pili, nakushukuru wewe kwa kunipa nafasi hii, lakini cha tatu nikupongeze sana kwa umahiri wako, ujasiri wako wa kukalia Kiti hicho. Kwa sababu hawa wenzetu wao mpaka sasa hivi kitu kinachowatoa humu ndani ni wewe siyo kwa sababu labda umewafanyia kitu kibaya ni kwa sababu umefuata kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mshairi mmoja anasema, mpewa hapokonyeki, aliyepewa akapewa. Wewe ukifanya chuki bure unajisumbua. Mola ndiye atoaye, mambo yote kamiliki. Kwa yule amtakaye ambaye humbariki na yule asiyemtaka basi kupata hatodiriki. Kwa hiyo, hawa wao watasema nje lakini wewe hapo umekaa umetulia kama jina lako lilivyo. (Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Naibu Spika, cheo ni jaha na jaha anayetoa ni Mungu. Jaha mpaji ni Mungu binadamu hana lake. Sasa wao kwa upande wao wanalia na hii jaha ya cheo na jaha hii ambayo mtu akipewa na Mungu, hata shetani alipopewa Nabii Adam, Mwenyezi Mungu anahadithia kwenye vitabu vya dini, anasema kwamba alivyowaambia malaika wamsujudie Adam, walisujudu isipokuwa ibilisi. Ibilisi yeye alikataa halafu akafanya kiburi. Kwa hiyo, wanachofanya hawa ni kiburi tu. Ibilisi akafukuzwa mbinguni akaambiwa toka, akatoa ahadi kwa Mungu nitakwenda huko ardhini kuwaposha waja wako. Hawapo huku, sasa wako Kahama, Mwanza, kwa ile ahadi yao kwamba watakwenda kuwapotosha Watanzania. Watanzania tunawaomba wawaelewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kumaliza uchaguzi tuliambiwa kwamba siasa zimehamia Bungeni kama wanavyozungumza watu wengine lakini sasa tazama, majimbo yale ya Wapinzani kule meupe, wote hawapo humu ndani. Hii ni sawasawa na hadithi moja ambayo niliwahi kuhadithiwa na wazee wangu kule, hadithi hiyo inazungumzia habari ya fensi ya ndoa. Katika fensi ya ndoa kuna bibi harusi huyo akipanda mumewe kitandani anatoka, akiingia mumewe chumbani katoka, kwa sababu anaogopa hajajiandaa na harusi, kwa hiyo watu wawaelewe. Kwa hiyo na hii iliyokuwa humu ni fensi ya ndoa, unapoingia watu wanaondoka, kwamba bibi harusi anamwogopa bwana harusi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni-conclude maneno kuhusu hawa, tusiwasemeseme sana kwa sababu kuna mshairi mmoja wa kiarabu anasema, Al junun funun alwak khalfan waheed. Wenda wazimu una matawi mengi sana na matawi ya wendawazimu hawa wenzetu wameyadandiadandia tumeyaona. Kwa hiyo, haya yote wanayokuja nayo, wameshakuja nayo mengi na hili moja katika matawi ya wendawazimu ambayo wamedandia. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa wenzetu ndiyo hatuwaoni humu Bungeni lakini sisi tutajadili kwa niaba yao. Sasa nije katika kuchangia bajeti yetu hii. Matumizi ya Serikali siku zote huwa yanapangwa kwa fedha. Fedha zinazopangwa badala yake huwa tunatazama yale mambo yaliyotarajiwa kwenda kufanyika lakini mambo yanayotarajiwa kwenda kufanyika tunatarajia yatokezee kwa 100%. Inawezekana fedha zikatumwa 100% lakini kazi isifanyike kwa 100% kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa gap hii tutaijua au itazibwa kutokana na ukaguzi unaofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Kwa hiyo, kuna kila umuhimu wa kuwa na taasisi hii ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Madhara yake kama itakuwa ukaguzi haukutosheleza ina maana kwamba mwaka unaofuata wa fedha tunaweza tukapeleka fedha tena katika miradi ileile na fedha ile isiweze kufanya kazi vizuri kwa sababu haiangaliwi, kwa hiyo, hili ni jambo muhimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zilizotengwa katika ofisi hii ni ndogo na nasema ndogo kwa sababu gani? Fedha zilizotengwa mwaka jana katika hizo OC, sizungumzii mishahara na development, nazungumzia OC za kufanyia kazi zilikuwa ni shilingi milioni 49 lakini mpaka kufikia Machi, 2016 fedha zilizotoka ni shilingi milioni 39, lakini fedha zilizotengwa kwa ajili ya mwaka huu wa fedha ambao tunaujadili hapa ni shilingi milioni 18.5 ya Other Charges. Shilingi milioni 44 humo kuna development na P.E. Kwa hiyo, hizi fedha tuna-justify kwamba ni kidogo kwa sababu ni asilimia 37 ya fedha zilizotoka mpaka Machi. Kwa hiyo, ukija kutazama kwamba zinatarajia kufanya kazi kwa mwaka mzima tutakuja kuona upungufu wa fedha hizi ni kiasi gani. Najua Serikali itakuja na mid year review lakini katika mid year review hili nalo tulione kama ahadi ya Serikali ilivyosema. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna kitu kimoja ambacho ni kizuri. Audit inapofanyika ina stage nyingi, kuna stage ya planning. Katika stage hii ya planning auditor anapanga wapi atafanya audit ile, anapanga resources, anapanga expert’s watakaohitajika wa-audit eneo fulani lakini pia anapanga na time consuming ambayo atatumia. Sasa katika hatua hizi za mwanzo auditor anahitaji kufanya hayo mambo kama resources zitakuwa hazitoshi ina maana kwamba ingekuwa ana-audit private office siyo Ofisi ya Serikali asinge-accept hii engagement kwa sababu resources zisingemtosheleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kingine muhimu katika kufanya audit, auditor wetu ana heshima kubwa sana Kimataifa. Katika kulinda reputation yake Kimataifa ni lazima auditor wetu afanye kazi vizuri na apelekewe fedha za kutosha ili aweze kufanya kazi kwa umakini na umahiri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia bajeti ya maendeleo ni kubwa, imeongezeka kwa asilimia 100. Kwa hiyo, tunatarajia fedha za maendeleo zikakaguliwe kwani zimeongezeka kwa asilimia 100. Kitu kingine Halmashauri zetu zimeongezeka kutoka 100 na zaidi hadi kufika 181. Ina maana kwamba kuongezeka kwa Halmashauri ni indication kwamba hata fedha za audit zingeweza kuongezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, isitoshe, tumesema kwamba Serikali imeamua kulipa madeni, lakini kabla ya kulipa madeni hayo inayakagua ili kupitisha kwamba deni gani linafaa kulipwa. Kwa hiyo, madeni haya ya Serikali yanayokaguliwa pia nayo yataongeza kazi ya auditor kwa hiyo ilipaswa fedha za auditing ziwe nyingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Serikali imeamua kufuta retention, makampuni ambayo yatafutiwa retention yatakuwa hayako radhi, hayataweza ku-submit kila kitu kikawa kiko safi. Kwa hiyo, Serikali ilipaswa iangalie suala hili ili Auditor General aweze kufanya mambo hayo ya ukaguzi. Pia taasisi kama Mahakama ya Kuzuia Ufisadi, TAKUKURU, Bunge tunategemea taarifa za CAG ili tuweze kufanya kazi. Kwa hiyo, hivi vyombo vinaweza vikakosa taarifa ya thamani katika kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kingine nije katika deni la Taifa. Wengi wamezungumzia deni la Taifa lakini deni la Taifa ni himilivu tunakubali lakini tunasema hivi, tukope tufanye zile kazi tulizoziainisha na tumalize kazi zile tulizokopea. Kama hatukumaliza, project zikiganda katikati interest rate inalipwa ina maana kwamba tunalipa fedha zetu au tumelipa fedha zimeganda, wananchi wanalipa interest na miradi inakuwa haijakamilika. Kwa hiyo, naomba suala hili tuweze kuliangalia vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini eneo lingine ambalo naweza kuchangia ni eneo la Bodi ya Taifa ya Ukaguzi ambayo ilitajwa katika Mpango. Bodi hii ya Taifa ya Ukaguzi tukifuata nchi za wenzetu huwa wanazitumia Bodi zao za Wahasibu na Auditors ili kuweza kutoa hata mitaala ya sheria za kodi ambazo zimetoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na yote, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)