Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa hisani hii. Kwanza kabisa naomba niseme nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Engineer Lwenge na timu yake kwa kazi nzuri ambayo amefanya, kitabu chenyewe kinajieleza, naunga mkono hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama mwanamke naomba nisimame nizungumze kama Mwenyekiti na samahani kwa hili kama wewe na wenzako mtaona haifai, lakini naamini kama wanaume mngekuwa mnateka maji, tungekuwa tumeshaondokana na tatizo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hapa tunaposimama leo kuzungumzia suala la maji tunazungumzia pia ajenda ya ukombozi wa mwanamke jamani! Miaka 55 baada ya uhuru huko vijijini hali ni tete na wote tunafahamu. Kwa hiyo, nafikiria hapa tukiangalia kazi nzuri ambayo iko mbele yetu, sasa mikakati ya kuanza kusambaza maji, watu wamezungumza hapa kimkakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumze kimkakati kwa sababu muda sio rafiki. Ni kwamba ili tuweze kuwafikishia Watanzania huduma hii ya maji maana maji ni huduma, lakini sasa hivi imekuwa biashara na biashara hiyo wanaonunua maji ni wanawake, ndoo ya maji inaweza hata ikafika sh. 1,000/= au sh. 500/=, kama huna mahali pa kuchota maji inabidi ununue maji. Kwa hiyo, unakuta kwamba mzigo wa mwanamke unazidi kuongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kabisa, kwanza namshukuru Mheshimiwa Waziri, nimeona katika Ibara ya 253 ya hotuba hii anazungumzia ushiriki wa sekta binafsi. Nataka kusema kwamba, juhudi za Serikali ni nzuri lakini suala hili ni gumu, hata tungeunda wakala wa maji jambo ambalo nalo linafikirika na wengi wamechangia bado utakuta kwamba Serikali peke yake haitaweza kuwafikishia Watanzania maji kwa haraka tunayoitaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Sekta binafsi, Mheshimiwa Waziri nadhani atakaposimama labda angetuambia afafanue kidogo jinsi anavyopanga kushawishi sekta binafsi kushirikiana na Serikali na halmashauri zetu katika kusambaza maji kwa haraka zaidi, hili jambo ni muhimu sana. Kule kwangu Muleba Kusini ambao ndio wajibu wangu hapa, nimeangalia Mheshimiwa Waziri bajeti na mpango aliotupangia nasikitika kusema kwamba haitoshi kabisa. Ninaposikitika hivi nadhani na wengine wengi humu ndani wanasikitika. Ndiyo maana angekuja basi na mkakati wa kutukomboa sisi akatuonesha jinsi tunavyoweza kutafuta wawekezaji kwa sababu maji mwisho wa siku watu wanachangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini uwekezaji katika maji huu unahitaji pia Serikali iangalie, ni lazima bei ziwe zinaweza kulipika. Kwa hiyo, sasa hivi nafikiria kwamba suala hili lingetusaidia sana. Kwa hiyo, katika miradi yako ya umwagiliaji Muleba, nasikitika kusema kwamba, miradi iliyowekwa awamu zilizopita fedha hiyo ni kama ilipotea, hakuna mradi unaofanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.