Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kukushukuru, lakini nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri.
Niende moja kwa moja katika Wizara hii ya Maji, nadhani umefika wakati sasa Serikali ijielekeze na ielekeze nguvu zake zote pale. Nimeona wametutengea shilingi bilioni mbili point nne, niombe sana kama walivyoomba wenzangu kwamba, fedha hizi sasa ifike wakati zije zote, ili tuweze kukamilisha miradi yetu ya maji iliyoko pale katika Jimbo la Singida Mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niishukuru Serikali kwa mradi wa maji mkubwa ambao uko pale katika Kata yangu ya Mwankoko. Changamoto kubwa iliyopo pale, mradi ule uko pale, lakini wananchi wa Mwankoko hawafaidiki na ule mradi ulioko pale. Kama hiyo haitoshi, wananchi wale walipisha ule mradi kwa maana kwamba, sasa walipaswa kulipwa fidia; uthamini umefanyika mara ya kwanza zaidi ya milioni 800 hawakulipwa! Umekwenda umefanyika mara ya pili, sasa hivi tunazungumzia bilioni moja na milioni 500 hazijalipwa mpaka sasa! Nilitarajia kuziona kwenye makabrasha haya ambao Mheshimiwa Waziri ametuletea au kwenye kitabu hiki kwamba, shilingi bilioni moja point tano wananchi hawa sasa wanakwenda kulipwa fedha zao za fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimwombe Mheshimiwa Waziri wakati anakuja kuwasilisha awaeleze wananchi wa Mwankoko kwamba, watalipwa fedha zao lini, ili kuondokana na hii adha ambayo inaendelea sasa. Na unafahamu kabisa kuchelewa kulipa zaidi ya miezi sita maana yake unakoelekea sasa wafanye uthamini wa tatu tunaenda kuzungumzia shilingi bilioni tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini uko mradi mwingine wa maji ambao uko eneo la Kisaki unaitwa mradi wa ILAO. Kwa bahati mbaya sana pale nako kuna zaidi ya shilingi bilioni tatu wananchi wanatakiwa walipwe, kwa ajili ya fidia wamepisha mradi wa maji wa ILAO. Vimechimbwa visima viwili pale Kisaki, vile visima viwili kwa hali iliyoko sasa tunakoelekea maana yake wananchi watakosa maji! Kisima kimoja kilikuwa kinatoa maji cubic metre 250 kwa saa na sasa zinashuka mpaka zimeenda 170 kwa muda wa mwaka mmoja! Kwa mwaka mwingine unaofuata, miaka miwili maana yake wananchi wa eneo lile wanaotegemea maji ya Mradi wa ILAO watakosa maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, anapokuja ku-wind up lazima atueleze kwamba, kwa namna gani sasa wananchi hawa tunaweza kuwakomboa na hii adha ambayo inajitokeza kwenye hili eneo la Kisaki. Kwa sasa wananchi wa eneo lile hawafaidiki na ule mradi! Wanalinda mradi, wanalinda maji na visima vilivyoko pale, lakini wao hawapati maji! Niiombe sana Serikali ifike mahali iwaonee huruma wananchi ambao wamepisha eneo lile kwa ajili ya mradi wa maji na wao wafaidike na yale maji, lakini waweze kulipwa fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uko mfumo wa maji taka. Nimwombe Mheshimiwa Waziri, tunayo maabara ya maji, sasa hebu zipewe nguvu hizi maabara za maji zitusaidie kuchunguza kwa sababu tukiacha sasa mfumo wa maji taka huu ukaenda holela hatutakuwa na uhakika na maji ambayo tunayapata sisi kwenye eneo lile! Bahati nzuri tayari tumekwishakaa, tumeandaa mradi mzuri ambao umeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwa ajili ya mfumo wa maji taka, unahitaji fedha. Nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, tunahitaji fedha, sisi tumeshajiwekea utaratibu mzuri juu ya ule mfumo wa maji taka, ili tuondokane na hili tatizo ambalo liko pale katika Jimbo la Singida Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzangu wamezungumzia juu ya Wakala; Wakala wa Maji Vijijini nadhani ndiyo suluhu. Pia Waheshimiwa Wabunge wameonesha hapa Mheshimiwa Waziri fedha atazipata wapi, fedha hizi wameeleza kwenye mafuta, tuongeze pale kama wanavyofanya EWURA shilingi 50, tuweke 50 nyingine, lakini kama haitoshi wamekwenda kwenye simu! Wala hakuna tatizo hatuhitaji kulijadili jambo hili! Nimwombe Mheshimiwa Waziri aliweke mezani, fedha zipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, ninaporudi mimi kule Jimboni swali hili linakuwa swali gumu sana; wananchi wangu hawana maji, tumewatengea shilingi bilioni mbili point nne! Bilioni mbili hizi tunaomba zifike, ili tuweze kuzisimamia na hizi fidia ambazo nimezizungumza za Mwankoko naomba nazo pia ziweze kuletwa.
MWENYEKITI: Ahsante.