Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuchangia. Kwanza kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu aliyenifanya nisimame hapa kwa siku ya leo, pili nawashukuru wananchi hasa wanawake wa Mkoa wa Morogoro walioniwezesha kurudi tena hapa Bungeni. Nampongeza Rais wangu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Mawaziri wake. Nampongeza pia Waziri wa Fedha kwa mpango mzuri aliouleta mbele yetu, jambo muhimu naomba utekelezwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naongelea kuhusu daraja la Kilombero, nawapa pole wananchi wa Kilombero na Ulanga kwa tatizo hili lililowapata. Kutokana na tatizo hili naomba kwenye mpango wetu huu unaoendelea tuweze kulipatia kipaumbele daraja la Kilombero.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vipaumbele naanza na viwanda; Mkoa wa Morogoro ni Mkoa wa Viwanda, lakini kusema ukweli viwanda vingi vimekufa, imebaki sana Kiwanda cha Tumbaku. Kiwanda cha Tumbaku ni cha watu binafsi, lakini kinafanya kazi nzuri na kimeajiri sana wanawake, kwa hiyo, naomba kiangaliwe vizuri kwa matatizo ambayo yatakuwepo. Kiwanda cha Nguo na chenyewe kinafanya vizuri, kina matatizo madogo madogo kwa sababu mara nyingi huwa kinatumia kuni, kwa hiyo uandaliwe mpango uangaliwe kusudi waweze kutumia nishati bora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vingi vya Morogoro vimekufa, kwa hiyo naomba wale watu ambao wamechukua hivi viwanda waweze kuvifufua kama hawatavifufua wapewe notice ya kuvirudisha kusudi viweze kufanya kazi. Viwanda hivi tumesema kuwa kwenye mpango viweze kutumia malighafi ambazo zinapatikana hapa nchini na hasa viwanda vya kilimo, uvuvi pamoja na mifugo. Mambo haya yatapendeza kwa sababu yataweza kuinua kipato cha Mtanzania na kitaweza kutoa ajira hasa kwa akinamama pamoja na vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa maji, Mkoa wa Morogoro na hasa Manispaa, bado tuna matatizo ya maji. Miradi ipo ya Millennia lakini tatizo la maji bado liko hapa hapo, naomba MORUWASA pamoja na Serikali, Serikali yangu naipenda Mkoa wa Morogoro na hasa Manispaa, waweze kuwapatia maji kama nilivyosema kuwa Manispaa inakua na watu wanaongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Morogoro una mito mingi kama ninavyosema, lakini Wilaya nyingi zote, Mji mdogo wa Gairo, Mji mdogo wa Mikumi, Morogoro Vijijini na kwingine kote bado wananchi hawapati maji salama. Wanaoteseka sana ni wanawake, badala ya wanawake hawa ambao ni wazalishaji kutumia huu muda wote kuzalisha, hasa wale ambao ni wakulima wanatumia muda mwingi kutafuta maji. Kwa hiyo, nashauri kwenye mpango huu tuangalie suala la maji na sio Morogoro peke yake ni Tanzania nzima, wanawake wanateseka kutafuta maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira, hapa nasema sana ajira kwa upande wa vijana. Kulikuwepo na Mfuko wa Vijana, naomba kujua unaendeleaje kusudi vijana wanaohitimu kwenye Vyuo vyetu waweze kupata ajira na kutumia vizuri huo Mfuko wa Vijana. Kwa upande wa Morogoro tuna vyuo Vikuu vingi, ambavyo vijana wanahitimu, kwa hiyo naomba huu Mfuko uweze kuwekwa wazi pamoja na sekta zote ambazo zinaweza kutoa mikopo kusudi vijana waweze kuelewa, waweze kujiajiri na kuanzisha Kampuni zao wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa misitu; nchi yetu ya Tanzania hasa na Mkoa wa Morogoro misitu imekwisha, wanakata miti wanatengeneza mkaa. Naomba kujua nishati mbadala, wananchi waweze kuelewa kuwa watumie nini hasa? Kuna mpango huu wa kata mti panda mti, lakini nafikiri licha ya hivyo haujatiliwa maanani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sera hii ya agizo la kupanga miti milioni 1,500,000 kwa kila Halmashauri. Ningeomba mkakati uwepo wazi wa kuangalia ni miti mingapi ambayo inaendelea kukua baada ya kupanda, tusiwe tunasema takwimu tu badala ya kufuatilia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa mapato; ili nchi yetu iweze kuendelea naomba sana isimamie mapato ya ndani na mapato ya nje ili kusudi tuweze kupata fedha za kutosha kuendeleza nchi yetu. Kwa upande uanzishaji wa Mji wa kilimo (The Agricultural Center) ambayo itakuwa Mkulazi kwa upande Morogoro, naomba mpango huu uangaliwe wananchi hawa wa Morogoro Kusini watafaidikaje na huu mradi wa Agricultural Centre City ambao utakuwa Mkulazi, hasa kwa upande wa Wanawake na Vijana ili kusudi waweze kufaidika kwenye huu Mji wa Kilimo ambao utakuwa pale Mkulazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa reli ya kati; kama ni reli ya kati ya ujenzi naomba kweli iwe reli ya kati. Tunavyoelewa reli ya kati inaanzia Dar es Salaam, Tabora mpaka Mwanza, halafu Tabora mpaka Kigoma na michepuko mingine. Kwa hiyo, reli ya kati iangaliwe kujengwa kwa gauge ambayo imesemwa ili kusudi wananchi waweze kufaidika pamoja na mizigo iweze kupitiwa kwenye reli siyo kwenye barabara, kwa sababu ikipita kwenye barabara hii mizigo mikubwa inaharibu barabara zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Morogoro, pia tunatumia reli ya TAZARA, naomba iangaliwe kwa sababu kutoka Dar es Salaam kuja Kisaki, mpaka Ifakara, Mlimba, Tanganyika Masagati tunatumia reli hii na Mkoa wa Morogoro ni mkoa wa kilimo, reli hii ya TAZARA inafaa kwa kusafirisha mazao yetu yaweze kuinua Mkoa wetu wa Morogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa nishati; kama unavyojua Morogoro kweli ina vyanzo viwili vya nishati ambavyo ni Kihansi pamoja na Kidatu, lakini mpaka sasa hivi vijiji vingi vya Mkoa wa Morogoro havina umeme. Namshukuru Mheshimiwa Waziri Profesa Muhongo amejitahidi lakini bado hatujapata umeme wa kutosha, kwa hiyo naomba tuweze kuliangalia Mkoa wa morogoro tuweze kupewa umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ardhi; kwa upande wa kupima ardhi pamoja na umilikishaji, pamoja na kutoa hatimiliki. Mheshimiwa Waziri Lukuvi amejitahidi na ameanza vizuri, naomba aendelee kwa sababu upimaji wa ardhi unasaidia sana kupunguza migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija upande wa Morogoro kwa upande wa wafugaji na wakulima, kwa kweli tuna tatizo kwenye Wilaya zetu za Morogoro hususani Mvemero, pamoja na Kilosa, Morogoro Vijijini na Kilombero wote kwa pamoja, kwa hiyo, naomba tuweze kuiangalia hiyo kusudi tuweze kupima ardhi yote na kuwamilikisha wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kilimo; nikija kwenye upande wa kilimo, Mkoa wa Morogoro ni Mkoa wa kilimo na wanawake ndiyo wakulima kweli, asilimia 70 ya chakula inayotolewa nchini kwetu inazalishwa na wanawake, kwa hiyo, naomba upande wa pembejeo, kwa upande wa Serikali naomba huu mfumo unaotumiwa wa kutoa ruzuku uweze kuangaliwa kusudi uanzishwe mfumo mwingine kama itawezekana wa kuweka pembejeo mwaka mzima lakini kwa kuweka bei elekezi ambayo kila mkulima aweze kuipata kwa wakati wake anaotaka.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Maafisa Ugani; tuna Vyuo vingi vya LITA, vya LITI, Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, wanatoa Maafisa Ugani, ninashauri hawa Maafisa Ugani waweze kuajiriwa mara moja.
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa .
MHE. DKT CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.