Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KAPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Napenda nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kuteuliwa kuongoza Wizara hii, lakini nataka nikupe pole kwa kazi ngumu iliyoko mbele yako, kati ya wewe na wapiga kura wangu, wanaotegemea Mradi wa Maji Makonde, ambao upatikanaji wa maji badala ya kupanda umeporomoka. Tunapata maji asilimia 30 ukilinganisha na vijiji vingine au Wilaya zingine ambako wameshafika asilimia 65 vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaendelea Waziri hoja yangu ni kwamba wala hatutaki Tandahimba, Newala Mtwara kunakofika huu mradi, hatutaki hela za kuendesha mradi, tunataka hela za kukarabati mradi ili kuongeza uzalishaji wa maji. Mchango wa wananchi wanaotegemea mradi huu kwa Serikali kila mwezi ni mdogo sana, kwa sababu maji mnayotuuzia ni kidogo sana, hatuna tatizo la kuchangia maji kwa sababu tangu tulivyoaanza Makonde Water Corperation tulikuwa tunanunua maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ujumbe wangu siyo kupitisha mafungu ya kuwezesha uendeshaji wa Mradi wa Maji Makonde, hoja leo hapa utakapokuwa unamalizia kesho kutwa, ueleze nini Wizara yako inafanya kuongeza uzalishaji maji kwa Mradi wa Maji Makonde. Mheshimiwa Waziri wewe umefika kule lakini nataka kukuomba, Naibu Waziri alikuja juzi wakati mvua inanyesha, watu wa Tandahimba, Newala ni hodari kwa kuvuna maji, kila nyumba ya bati utakayoiona tunachimba kisima, tunavuna maji ya mvua, mimi naishi kijiji kwangu, sina maji ya bomba katika nyumba yangu, nina visima viwili, napata maji ya shower na ya kunywa kwa sababu tunachimba visima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wa Tandahimba na Newala kama wangelitegemea tu maji ya bomba ya Serikali hali yetu ya maisha ingekuwa ngumu sana. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri ninachoomba hapa siyo utueleze unafanya nini katika administration uendeshaji wa Mradi wa Maji Makonde, aaah aah! Utakapokuwa una- wind up utoe maelezo nini Wizara yako inafanya kuongeza uzalishaji wa maji katika Mradi wa Maji Makonde. Hiyo ndiyo hoja yangu, umri huu siyo wa kutoa shilingi, lakini kama hutatufikisha huko, kuna vijana wengine humu ndani wanategemea mradi huo huo mimi nitakaa pembeni huku nawapigia kwa chini chini (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji Makonde, Tatizo la maji Newala, Tandahimba ni kubwa kwa sababu ya jiografia, ile inaitwa Makonde plateau, niliposoma jiografia niliambiwa a plateau is arised flat peace of land. Plateau ni kitu gani, ni eneo ambalo limeinuka, na juu kuko flat ndivyo ilivyo uwanda wa Makonde ukija kwetu Tandahimba na Newala, ukienda Masasi, Mto Ruvuma, Lindi, Mtwara unateremka, ndiyo maana katika eneo la kwetu hatuna agenda visima vifupi haipo. The water table is so below unaweza ukachimba hata maili ngapi sijui, siku hizi mnatumia kilometa, unaweza ukachimba sijui kilomita ngapi hujapata maji, hatuna visima vifupi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia hapa the oldest scheme ya maji ambayo inaendeshwa na Taifa ni Mradi wa Maji Makonde, lakini naona tumepewa shilingi bilioni mbili. Shilingi bilioni mbili upeleke maji Tandahimba yaende mpaka Mtwara, mradi mwingine wa Kitaifa three hundred thirty thousand Euro, mradi mwingine twenty thousand billion, mradi mwingine three point; Mradi wa Maji Makonde shilingi bilioni mbili, Waziri naomba hili jambo ulitazame.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo sitaki kwenda katika historia, watu wa Newala - Tandahimba baada ya kuona shida zetu za maji ni kubwa, enzi ya mkoloni 1953 tulianzisha kampuni iliyokuwa inaitwa Makonde Water Corporation, kwa wazee waliokuwepo hisa ilikuwa shilingi 20 kampuni ikaenda kukopa hela Uingereza ikaanzisha Mradi wa Maji Makonde na mwaka 1954 mradi ukafunguliwa kwa sababu palikuwa na cost sharing kila mwaka tulikuwa tunapeleka maji vijiji vipya, maji yakawa yanapatikana bila matitizo every domestic point.
Baada ya mradi kuchukuliwa na Serikali kusema sasa hapana, tuachieni tunaendesha sisi tumerudi nyuma. Nimekaa Bungeni hii term ya tatu, nilipoingia upatikanaji wa maji Newala ulikuwa 22 percent miaka yangu kumi ya kufurukuta pamoja na uzito niliokuwa nao tumeongeza asilimia nane tu. Kama miaka kumi asilimia nane mpaka tufike hiyo asilimia 65 itatuchukua miaka mingapi? (Makofi)
Mheshimiwa Waziri ninachotaka kusema Mradi wa Maji Makonde una matatizo makubwa yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo hayo ni pamoja na uchakavu wa mitambo, mabomba yale enzi ya mkoloni hayakuwa plastic yalikuwa ni ya chuma yameoza yametoboka kwa hiyo maji yanayopotea njiani ni mengi. Hatuna pampu za kutosha, wataalam hawatoshi, vituo vichache vya kugawia maji, kwa ujumla uzalishaji mdogo wa maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waziri utakapokuwa unajibu narudia tena ueleze mwaka huu Serikali inafanya nini kuongeza uzalishaji wa maji Makonde, nakuomba uje kiangazi, Waziri wako alikuja wakati wa masika hakuona shida ya watu, wakati wa masika ndoo moja ya maji shilingi 1,000!
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi mingine ndugu yangu pale Mheshimiwa Bwanausi ameelezea, mradi wa maji Chiwambo ulikuwa unafika mpaka Newala hauji tena, Mradi wa Maji wa Luchemo tulipata mafuriko mwaka 1990 mashine zile zikasombwa na maji tangu 1990 mpaka leo hakuna replacement. Mheshimiwa Waziri naomba sana fufueni Mradi wa Luchemo tuunganisheni watu wa Newala na Mradi wa Chiwambo kwa ndugu yangu Mheshimiwa Bwanausi na ninashukuru ameuzungumzia hapa, naomba sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kwamba tunapata taabu Viongozi, mradi wa maji wa Kitangari – Mitema, Mji mdogo wa Kitangari upo kilomita tatu kutoka pale, hawapati maji. Maji yale ya Mitema yanasukumwa yanafika mpaka Tandahimba, hapa kwenye source ya maji hawapati maji.
Mimi mnanipa taabu sana maana inabidi niwabembeleze wapiga kura wangu, wanataka wapige shoka maji yale ili tukose wote, nawaambia hapana subirini Serikali inachukua hatua, sasa mwisho nitaitwa muongo, hivi umri huu na mvi hizi niitwe muongo Mheshimiwa Waziri unafurahi? Hivyo, tuaomba tatizo la maji la Mji Mdogo wa Kitangari lishughulikiwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo sugu ambalo watumishi wa maji Newala hawataki kusikia. Tumepitisha maazimio kwenye Halmashauri, marufuku kupeleka maji katika visima vya watu binafsi, palekeni maji katika domestic point za public pale ambapo kila mmoja anapata maji. Maafisa wako wanachofanya wanapeleka maji katika nyumba za watu binafsi, wanawajazia maji baadae wale wanawauzia wananchi maji ndoo shilingi elfu moja, ukiwaambia kwa nini hampeleki katika domestic point ambayo watu wote tunapata pale hawana majibu! Jawabu nini corruption. Hebu Waziri tamka kesho kutwa utakapo wind up na uwaagize watumishi wa maji Newala kwamba….
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja nakutakia kila la kheri mdogo wangu unijibu vizuri kesho kutwa. Ahsante.