Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hotuba ya Bajeti ya Wizara yako kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la maliasili ni pamoja na Hifadhi za Taifa (TANAPA), bahari, mito, misitu na mbuga za wanyama au hifadhi. Tanga tunazo mbuga au hifadhi kama Mwalajembe, Kalalani, Mkomazi na Saadani, lakini bado hazijatangazwa katika medani za kitaifa, kiasi kikubwa cha kutosha. Naiomba Wizara yako ihakikishe inazitangaza mbuga za Mkomazi, Mwakijembe, Kalamani na Saadani katika viwango vya kimataifa ili ziweze kujulikana na kutembelewa na watalii wa ndani na nje na kuingiza mapato ya fedha za kigeni (foreign currency).
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanapokuja watalii ajira zinaongezeka, kutajengwa hoteli, zitaajiri wahudumu pia wasafirishaji maliasili, pamoja na misitu. Napenda kuzungumzia utunzaji wa misitu ya nchi kavu na baharini pembezoni mwa barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo ambayo kuna shughuli za utalii au maliasili na ikiwa kuna mapato yanaingia asilimia 20 zirudi katika eneo husika. Ikibidi isiwe fedha, ziwe samani au vifaa kama madawati, ujenzi wa zahanati na kadhalika. Naomba Tanga Mjini isikose madawati ya TANAPA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumezuka tabia ya kuibiwa wanyama pori wetu, ndege wetu na viumbe hai na kupelekwa nchi mbalimbali za Ulaya, Marekani na Asia, je, ni akina nani wanaofanya biashara hii haramu? Lazima nchi idai rasilimali zake na itunze viumbe hai hawa na anayehusika akipatikana hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.