Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uokoaji katika Mlima Kilimanjaro bado huduma ya uokoaji siyo nzuri. Gari halifiki kwenye high altitude na tunapoteza maisha ya watu huko mlimani, kwa nini TANAPA wasinunue helkopta ambayo inaweza kuokoa watu na wagonjwa kwenye high altitude? Hii inaweza kutumika kwenye park zote kwa ajili ya uokoaji pia kulinda majangili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake waliopo half mile katika Mlima Kilimanjaro wananyanyaswa sana, wanapigwa na askari wanaolinda msituni, wanafikia hata kubakwa. Ikumbukwe kuwa wao ndiyo wanaolinda mlima, wanatumika kuzima moto unapowaka, wanasaidia watu wasikate miti na pia watu hutumia njia ili kwenda nyumbani. Kuna kijana alipigwa risasi akielekea nyumbani kutoka Kibosho anaitwa Kiwale, je, kesi yake imefikia wapi? Copy nimempa Mheshimiwa Waziri kwa reference.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Umbwe route katika Mlima Kilimanjaro, route hii ni nzuri sana lakini Umbwe cave hakuna maji wala choo, watu wanajisaidia kwenye misitu, hii ni aibu wakati wageni wanalipa kuingia kwenye hifadhi, ni kwa nini wasifuatwe walipe forest fees na park fees wakati park ni moja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine Umbwe route hakuna walinzi wa msituni na ukizingatia camp hii ipo karibu kabisa na Kibosho. Umbwe kwa wana vijiji ni rahisi watalii kuvamia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, route ya Old Moshi tayari Wizara ya Miundombinu imetenga fedha kwa ajili ya kutengeneza barabara kutoka Kiboriloni, Kikarara, Kidia, mpaka Tsuduni na njia hii ni fupi kufika Uhuru Peak, kuna water falls na vipepeo, sasa ni lini route hii itaanza kazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na wimbi la wazungu wanaojitokeza ku-volunteers kuja kufanya kazi, lakini sasa hivi wanachokifanya wanafanya biashara ya utalii na wanawalaza wageni majumbani katika mitaa ya Moshi, Soweto Rau na kadhalika, wanatumia biashara ya mlima bila kulipa kodi, nashauri tour operaters wote kuwe ni lazima wapeleke TALA licence na tax clearance ili kuonyesha wanalipa kodi. Hii itafanya kodi nyingi kukusanywa na itakuwa ngumu kubakiza fedha nyingi Ulaya.