Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kwenye maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuimarisha utalii katika nchi yetu, nchi yetu ina vivutio vingi kama mbuga za wanyama, Mlima Kilimanjaro, maziwa na masalio ya kale. Serikali iongeze matangazo nchi za nje ili kuvutia watalii wengi zaidi pia usalama na amani ya nchi ni muhimu sana kuongeza hoteli na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna misitu mingi ambayo lazima ilindwe na kuvuna kwa utaratibu mzuri, haiwezekani nchi kukosa madawati katika shule zetu. Kuna wananchi wengi hasa katika maeneo ya Nanyara, Songwe na kadhalika wananyanyaswa sana na maliasili. Wengi wanapanda miti ambayo wanakata ili kuchomea chokaa, cha ajabu wanatozwa shilingi 15,000 kwa mti mmoja bila receipt naomba mfuatilie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kimondo cha Ndolezi Mbozi ni muhimu kikajengewa fence ili kukihifadhi na kuimarisha utalii katika eneo hilo ni muhimu sana.