Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza na kuunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Waziri kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na Katibu Mkuu kwa kazi kubwa wanayoifanya. Mchango wangu utakuwa katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utalii wa mambo ya kale ya kihistoria, maeneo mengi ya kihistoria yametelekezwa, hayana maendeleo yoyote. Yapo baadhi ya maeneo yamesambaratika kabisa. Maeneo ya kihistoria iwapo yanaboreshwa na kutengenezwa vizuri yangeweza kuleta mapato makubwa kwa Taifa letu. Tunaenda katika nchi kama China watu walio wengi wanaenda kuangalia Great Wall. Serikali inapata fedha nyingi sana lakini India pia kuna Taj Mahal wanaingiza watalii wengi sana. Je, Tanzania tumejipanga vipi katika kutangaza maeneo yetu ya kihistoria badala ya kutegemea utalii wa mbuga peke yake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali waangalie utalii wa kihistoria na tutangaze maeneo hayo ya kihistoria, matangazo ya utalii hayaonekani katika viwanja vya ndege, maeneo ya bandari na stendi kuu za mabasi. Waongozaji wetu wa watalii walio wengi wako Mkoa wa Arusha na maeneo ya Dar es Salaam na Bagamoyo siyo wengi sana. Lakini ma-tour guide wetu wanazidiwa na wale wa Kenya, Serikali imejipangaje katika kuwajengea uwezo watu wetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, msitu wa Mwandege na misitu mingi iliyopo Mkoa wa Pwani imekuwa ni makazi ya majambazi na wezi. Serikali imefanya vizuri sana kutenga maeneo ya misitu kwa kusaidia kutunza mazingira na kuhifadhi ardhi kwa matumizi ya baadaye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Dar es Salaam sasa idadi ya watu imeongezeka kwa kiasi kikubwa sana, Mbagala imejaa watu wanaelekea Mkuranga, msitu wa Mwandege uko katikati umezungukwa na makazi ya watu, watu wanaingilia hifadhi na Serikali hakuna wanachosema hatma yake ni kuwabomolea nyumba zao kwani wakati wanajenga Serikali ilikuwa wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itoe baadhi ya eneo la Msitu wa Mwandege wawape Halmashauri ya Temeke watengeneze kituo kikubwa cha mabasi ya Mikoa ya Kusini na eneo linalobaki liendelezwe kama msitu na litunzwe kwa manufaa ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu tozo za mazao ya misitu. Gharama za kupitisha kitanda kimoja kutoka Mkoa wa Pwani kwenda Dar es Salaam ni kubwa kuliko ulizonunulia kitanda kijijini. Lakini fedha hizi wanazokusanya kweli zinaenda Serikali? Kwa kuwa tunasikia wafanyakazi wa vituo hivyo walio wengi siyo waaminifu ni vema sasa Serikali ikaangalia nidhamu na uadilifu wa wafanyakazi wa vituo vya ukaguzi wa mali na misitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.