Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la majengo ya kale (Miji Mikongwe); Tanzania tunaongeza pato la nchi kwa utalii kwa sababu tuna vivutio vingi lakini Serikali yetu inashindwa kukarabati baadhi ya vivutio kama magofu ya kale yaliyopo Bagamoyo, Kilwa na kadhalika. Ni lazima Serikali ikarabati magofu haya ili tuweze kuongeza mapato ya nchi katika sekta hii ya utalii ili wananchi waweze kunufaika kwa kupata ajira.
Mheshimwa Mwenyekiti, ni lazima Serikali itenge bajeti ya kutosha kukarabati magofu haya ya kale. Mji wa Bagamoyo ni kivutio kikubwa sana kwa watalii. Maeneo ya Bagamoyo na Zanzibar yametaka kufanana ramani ya Mji Mkongwe Bagamoyo imeanza kupotea kwa sababu wananchi wanauza maeneo hayo na wafanyabiashara wananunua maeneo haya na kujenga majengo mapya na kuondosha vivutio vya watalii. Serikali isipodhibiti hali hii ya uharibifu wa vivutio vya utalii tunaweza kupoteza vivutio vya utalii kwa miaka ya mbele na kukosa watalii katika Mji wa Bagamoyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vituo vilivyokuwa vikipitisha watumwa (bandari) zimesahauliwa na bandari hizi ni vivutio kwa watalii. Baadhi ya watalii wanapofika Zanzibar ni lazima waende na Bagamoyo kwani Bagamoyo ni kivutio kikubwa kwa watalii. Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti majumba ya Mji Mkongwe wa Bagamoyo ambapo wananchi wamekuwa wakibomoa na kujenga majengo mapya na kupoteza ramani ya Mji Mkongwe. Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya kutosha katika sekta hii ya utalii na kukarabati maeneo ya Mji Mkongwe ili tuzidi kuongeza Pato la Taifa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la hoteli za kitalii; Tanzania tuna hoteli nyingi za kitalii lakini Watanzania wamekuwa wanapata shida wanapoenda kuomba kazi katika hoteli kwani wanaopewa kipaumbele ni wageni kutoka nchi jirani na siyo Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya wawekezaji wanaowekeza katika sekta ya hoteli wanapokuwa wamekodi hoteli wakishindwa kulipa kodi wanabadilisha majina ya hoteli hizo au hao wawekezaji wanawakodisha watu wengine na kubadilisha majina ya hoteli kwa kukwepa kulipa kodi. Wawekezaji wakija kuwekeza katika sekta ya hoteli ni lazima Watanzania wapewe kipaumbele kwani kuna vijana wengi hawana ajira na wana uwezo wa kufanya kazi hotelini.
Je, Serikali imejipangaje kudhibiti ukwepaji wa kodi katika sekta hii ya hoteli za kitalii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Balozi zetu kutangaza utalii; nchi za wenzetu wamekuwa wakitumia Balozi zao kutangaza utalii. Kwa sababu sisi tuna vivutio vingi kuliko hizo nchi za wenzetu kama tusipotangaza utalii wetu ipasavyo hatutoweza kupata watalii wa kutosha. Kwa mfano ukitoka na ndege Uingereza ukifika Kenya watalii wengi wanashuka kiwanja cha ndege cha Kenya. Kwa maana hiyo Kenya wametuzidi kwa kutangaza utalii. Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya kutosha kufanya matangazo ya vivutio vyetu vya utalii nje ya nchi?