Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa ujumla kwa utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi. Mchango wangu utajikita katika mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ndogo ya wanyamapori/migogoro ya mipaka katika marejeo ya Sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009; Serikali ilielekezwa kutathmini juu ya uendelezaji wa mapori ya akiba na mapori tengefu yote yaliyoko nchini ili kubaini uendelezaji wake, aidha, marekebisho ya mipaka yake ili kuondoa migogoro ya ardhi baina ya mapori hayo na ardhi ya vijiji vinavyopakana navyo, hadi leo maelekezo hayo ya Bunge bado hayajatekelezwa na Serikali na badala yake ni kuendelea kwa migogoro katika mapori hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la migogoro ya aina hii hususan kwa pori tengefu la Kilombero na vijiji jirani, nimeliongelea sana na mara ya mwisho Serikali kupitia Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu, Aprili, 2014 alitoa agizo kwa Wizara ya Maliasili kuweka utatuzi wa kudumu katika mgogoro wa ardhi kwa pori hilo na mengine lakini hadi leo agizo hili halijatekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha hoja yake atoe kauli ya wazi, ni lini ardhi iliyoko katika eneo la buffer zone katika pori tengefu la Kilombero itarejeshwa katika ardhi ya vijiji ili iweze kutumika kwa matumizi ya kilimo na mifugo ambayo ndio uhai wa wananchi hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani na nitaunga mkono kama Waziri atatoa majibu ya kuridhisha katika ombi la wananchi wa Ulanga na Malinyi.