Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kuipongeza Wizara hii ya Maliasili na Utalii kwa kazi nzuri wanayoifanya wakiongozwa na Profesa Jumanne Maghembe pamoja na watalaam wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri na yenye ubora wanayoifanya katika kulinda maliasili ya nchi yetu, ambacho ni kivutio cha utalii ndani na nje ya nchi yetu Tanzania na ndicho kichocheo cha maendeleo ya Taifa letu. Natambua Wizara hii ni ngumu na ina changamoto nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara hii itazame vizuri kwenye maeneo ya mipaka ya Hifadhi ya Wanyamapori (game reserves), kwani kumekuwa na malalamiko makubwa kwa Maafisa wa Wanyamapori ikiwa ni pamoja na vitendo vya uovu kwa wananchi kwa kuwatoza faini zisizo kwenye utaratibu wa kawaida wa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Maofisa wamekuwa wakiwaswaga ng‟ombe na kuwaingiza ndani ya hifadhi hata kama watakuwa nje ya hifadhi. Nashauri Serikali kupitia Wizara hii iweze kutatua kero hii kubwa inayosumbua wafugaji wengi hapa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.