Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuendeleza maliasili zetu na watalii wanaoingia nchini mwetu wanaongezeka siku hadi siku. Ni jambo jema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kama tutajipanga vizuri kwa kuutangaza utalii na vivutio tulivyonavyo, mapato yetu yanayotokana na utalii yataongezeka zaidi. Mfano, utalii wa viungo; tuwahamasishe wananchi wetu kupitia mtu mmoja mmoja au vikundi kuanzisha mashamba ya viungo (spices) mbalimbali na watalii wataona kitu kingine badala ya wanyama pekee na wananchi wataongeza vipato vyao moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kuwaandaa wananchi kuvutia watalii kwa utamaduni wetu wa asili, mfano ngoma zetu za asili, mila na desturi zetu za asili, mavazi, chakula, lugha, malezi na kadhalika. Kwa utalii wa historia utahusu watawala waliopita na kutawala.