Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kuhusu suala la utalii wa Zanzibar. Utalii wa Zanzibar wageni wengi wamepungua kwa sababu mbalimbali za kisiasa na mengineyo. Sasa naomba Serikali ya Tanzania Bara iweze kusukuma utalii huu wa Zanzibar ili kupata nguvu kama utalii wa Tanzania Bara na wananchi wengi wanategemea utalii hususan vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni mapato. Hii tozo inayotokana na utalii ikusanywe vizuri ili Zanzibar iweze kupata mapato vizuri. Kama ilivyoelezwa katika ukurasa wa 88 kuwa tufahamu wageni wanaingia na kutoka. Hiyo tozo inayopatikana ni kiasi gani ili wananchi wa Zanzibar waweze kufahamu, kwa mwaka mapato yanayopatikana, ili kusukuma maendeleo ya Zanzibar yatokanayo na utalii.