Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ifute hifadhi ambazo hazina wanyama tena na maeneo hayo yagawiwe kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali isisitize kwa mabalozi walioko nchi za nje kufanya kazi kwa ukamilifu kutangaza vivutio vyetu na kuwe na library zao za maliasili yao katika ofisi zao zinazoelezea jinsi Tanzania ilivyo ikiwa ni pamoja na tamaduni zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoteli za Tanzania ziboreshwe, pia kuwepo na vyuo vikuu vya kufundishia wahudumu wa hoteli hizo Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, misitu ni mali, Serikali ijipange kupanda miti, pia kutoa zawadi kwa kushindanisha wapandaji bora, waweza kuwa ni Taasisi kwa Taasisi au Wilaya kwa Wilaya.