Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kupongeza kwa hotuba nzuri iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri. Pia napongeza kwa kazi inayofanyika ndani ya Wizara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto yangu ipo katika mipaka kati ya vijiji vinavyozunguka misitu ya hifadhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Jimbo la Busanda katika kijiji cha Saragulwa; kuna mgogoro wa mara kwa mara baina ya hifadhi ya msitu wa Geita na kijiji cha Saragulwa. Mgogoro huu unasababisha kero kubwa sana kwa wananchi waishio katika kijiji kutokana na adha za kutaka kuchomewa nyumba na kufyeka mazao ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kupitia Wizara ione umuhimu wa kuangalia upya mipaka yake na kutoa elimu kwa wananchi juu ya mipaka hiyo na kuwaeleza bayana adhabu zinazotokana na kukiuka mipaka iliyowekwa.
Kijiji cha Saragulwa kimekuwepo tangu Azimio la Vijiji vya Ujamaa na kinatambulika TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni juu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kutokuwa na Bodi. Hii ni changamoto kubwa katika utendaji wa shirika na tunakosa mapato kwa kutokuwa na Bodi. Nashauri Serikali ifanye utaratibu wa kupata Bodi mpya haraka iwezekanavyo ili kunusuru hasara tunayoipata kwa kukosa mapato kwa wakati (concession fees).
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, naipongeza TANAPA kwa kutoa madawati kwa Wilaya mbalimbali hapa nchini. Hata hivyo, naomba TANAPA ituangalie Wilaya zenye changamoto kubwa ya watoto kukaa chini. Natumia fursa hii kuiomba TANAPA mchango wa madawati katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Tuna changamoto kubwa sana, tunaomba support.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, mwisho liko tatizo la mamba katika vijiji vinavyozunguka Ziwa Victoria hasa katika vijiji vya Kasangalwa, Kageye, Bukando na Chankorongo. Mara kwa mara kunatokea matukio ya wananchi kuliwa na mamba. Naiomba Serikali ilifanyie utatuzi kwa haraka kwa sababu tunapoteza nguvu kazi ya Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuwa Wizara itayafanyia kazi matatizo yote niliyoyawasilisha. Naunga mkono hoja.