Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja. Jimbo la Nkasi Kusini lina mbuga iitwayo Rwamfi Game Reserve. Katika mipaka ya mbuga hii kuna migogoro kati yake na vijiji jirani kwa Jimbo la Nkasi Kusini, vijiji vya King‟ombe, Mlambo, Kasapa, Ng‟undwe, Namansi na vijiji vya China na Nkata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vyote hivi vimekuwepo kabla ya kuanzisha Hifadhi hii, lakini wahifadhi wamekuwa wakidai kuwa wananchi wanaishi ndani ya hifadhi. Naishauri Serikali ije na mkakati mpya kuangalia kwa upya mipaka ya mbuga hii ili kuleta uelewano na vijiji jirani na kuondoa usumbufu unaotokana na wahifadhi kusumbua wananchi ikiwa ni pamoja na kuwapiga. Wananchi hawaelewi kwa nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi imevikuta vijiji hivyo vyenye haki na huduma zote za kijamii ikiwa ni pamoja na shule za sekondari, zahanati na vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la vijiji hivi halitoshi pia kwa shughuli za kuendesha maisha. Tunaomba sehemu ya mbuga hii ipunguzwe kutoa eneo la kilimo kwa kilimo zaidi.