Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hotuba hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na mgogoro katika Hifadhi ya Akiba ya Uwanda kutokana na ongezeko kubwa la watu waliopo katika vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo kwa sababu zifuatazo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi hiyo mipaka yake kutoeleweka, askari wanyama pori kutoza wafugaji fedha ili walishe mifugo yao ndani ya hifadhi; kukodisha ardhi iliyomo ndani ya hifadhi ili wakulima waweze kulima; askari wa wanyama pori kuruhusu wananchi wasio na uwezo wa fedha walime mazao yao na mazao yakishakomaa hutumia ujeuri wa kupora mazao yao wanayauza na kuingiza fedha hizo mifukoni mwao; kuwanyang‟anya pikipiki, baiskeli, majembe ya plau na majembe ya mkono, fyekeo, panga na kadhalika, jambo ambalo linahatarisha amani. Kama Serikali haitachukua hatua haraka ipo siku yatatokea mapigano kati ya askari hao na wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi hiyo kwa sasa haina sifa, ni hasara tu kwa Serikali, inawanufaisha Askari tu. Hivyo kutokana na uhaba wa ardhi, nashauri, hifadhi hiyo ipunguzwe au kufutwa kabisa, wananchi wagawiwe ardhi hiyo waendeleze uchumi wao kwa kulima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri anieleze nini faida ya hifadhi hiyo kwa Serikali na kwa wananchi hadi sasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri hifadhi ipunguzwe kama siyo kufutwa kabisa. Mipaka ijulikane, Serikali itoe misaada ya kuwajengea shule, zahanati na kuwapatia madawati ili kuwatia moyo wananchi. Pia nashauri Mheshimiwa Waziri atembelee eneo hili la hifadhi ili ajifunze na baadaye aweze kutoa uamuzi sahihi kuliko kusikiliza kwa mbali. Ahsante.