Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wake wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sana Wizara iongeze wigo wa utalii kwani sekta hii ni sekta muhimu yenye mchango mkubwa katika Pato la Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Makumbusho ya Taifa, taasisi hii ikiendelezwa na kusimamiwa vizuri ikaboreshwa zaidi inaweza nayo ikatoa mchango wake. Pale katika Kijiji cha Makumbusho (Millennium Towers) eneo ni kubwa, lingeweza kutengenezwa na kuendelezwa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze kwa namna tao la Mashariki (milima) inavyolindwa. Ombi langu endeleeni kuangalia milima hiyo ikiwemo Msitu wa Shengena. Naunga mkono hoja.