Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupata majibu kuhusu suala la mjusi (mabaki yake) ambayo yalichukuliwa Tendegu katika Jimbo la Mchinga na kupelekwa Ujerumani, naomba kupata majibu ya hoja zangu hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali inanufaika na nini kutokana na mjusi huyo kuhifadhiwa huko. Mheshimiwa Waziri hii hauoni kwamba suala hili linatuletea fedheha kubwa Watanzania kwa kuonekana kwamba hatujali na kuthamini rasilimali na maliasili za nchi yetu? Kwa nini rasilimali kubwa na ya kihistoria kama hii imebaki Ujerumani bila sisi kama Taifa kunufaika kwa chochote? Kumekuwa na kauli tata kuhusu manufaa ya mjusi huyu kutokana na suala hili pia kuihusisha Wizara ya Mambo ya Nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kuwasilisha.