Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kukosekana kwa mkakati madhubuti (strategic plan) wa kutangaza rasilimali na vivutio vyetu kunasababisha nchi nyingine kunufaika zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waziri mwenye Wizara husika wakati atakapokuja kuhitimisha hoja aje na mpango mkakati unaoelekeza kutoa fursa kwa taasisi au watu wenye uwezo ili waweze kutangaza vivutio na rasilimali zetu kimkakati zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inakuwa ni vigumu sana kuona ujangili katika nchi yetu unakuwa kwa kasi wakati kuna watumishi walioajiriwa kwa kazi ya kulinda wanyama, hata pembe za ndovu zikikamatwa mwisho wake zinapopelekwa hakujulikani, hata mrejesho wowote katika Bunge hili Tukufu ili kupata taarifa yoyote endelevu juu ya kesi endapo watuhumiwa wameshinda kesi wananchi kinyemela. Hii ndiyo sababu kubwa inayokuza kazi haramu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali isione vigumu kutoa taarifa muhimu kama hiyo katika Bunge lako Tukufu tena taarifa hizi zinapotolewa jina la mtuhumiwa litajwe kufanya hivyo hivyo ujangili utapungua.