Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na muda kuwa mdogo, ningependa kuongeza mchango wangu niliozungumza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwaombea wananchi 1,128 wa Derema wafikiriwe kuongezwa fidia, lakini bado hati ya shamba la Kibaranga tunapotegemea kuwahamishia haijapatikana, Waziri wa Ardhi anafahamu suala hili. Wizara ifikirie zaidi kuwaongezea vibali wanavijiji ambao wako karibu na shamba la Tiki. Wananchi hawa ambao ni vibarua wa shamba hilo la Derema wanalalamika kwa kupewa vibali vichache mno.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ifikirie kuanzisha Chuo cha Hifadhi ya Asili ambacho hakuna hapa Afrika Mashariki na Kati. Muheza tutakuwa tayari kutoa eneo la chuo hicho. Ili kuongeza watalii nchini, pamoja na kununua ndege tatu ambazo hakikisha kati ya hizo zilenge nchi zenye watalii wengi, ni vizuri kuongeza au kuwatafuta tour operators, ambao wanaweza kufungua ofisi hizo kwa wingi nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ifikirie kuboresha sehemu ya kituo cha Horombo ambacho ni njia ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Iboreshe kukuza utalii wa ndani ili kuwawezesha wananchi kufika hapo kwa kuwa magari yanafika na wengi wanaweza kufika na kuona milima yote vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, askari wanyamapori waendelee kupata mafunzo zaidi na waajiriwe wengi kukidhi mbuga zote.