Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi napenda nichangie kwa njia ya maandishi bajeti ya Wizara ya Maliasili kwa mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uteuzi wake kwa Profesa Jumanne Maghembe, Waziri mwenye dhamana Wizara ya Maliasili na Utalii. Mimi binafsi naamini shule na weledi wa Profesa Maghembe katika Wizara ya Maliasili na Utalii ni silaha nzuri katika ujenzi wa makuzi ya sekta ya maliasili na utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na pongezi hizi pia ningependa nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uteuzi wake wa Engineer Ramo Makani katika ujenzi wa sekta ya utalii. Mimi napenda kusoma vitabu vya Peter Senge ambaye ameandika masuala mengi ya management, ambapo moja ya michango yake aliweza kuonesha mahusiano ya kada za Injinia na best management practice.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nichangie kwa kujikita zaidi kwenye suala zima la mahusiano ya michezo na utalii. Moja kwa moja kwa uhusika wangu kwenye mbio za marathon zilizofanyika mapema mwezi Feburuari, 2016. Katika mbio hizo lipo jambo moja kuu la utangazaji wa maliasili kupitia michezo ambalo nilifikiri ni vyema tusilipuuzie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika marathon iliyofanyika mkoani Kilimanjaro ambapo Mheshimiwa Waziri wa Habari na Michezo alikuwa mgeni rasmi tuliona kwa pamoja namna ambavyo maliasili ya uoto wa Mlima Kilimanjaro unavyotumika na makampuni binafsi katika kujipatia vipato vya mtu mmoja mmoja. Katika marathon hii, napenda Bunge lako Tukufu limtambue Ndugu John Harrison mzaliwa wa South Africa ambaye ndiye aliyeandaa mbio hizi za marathon.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuonyesha masikitiko yangu makubwa katika maandalizi na uendeshaji wa mbio hizi za marathon. Mbio hizi zilizoshirikisha Mataifa ya nje, zaidi ya watu 30,000 na wazawa 70,000 hapakuwa na ushiriki wowote wa TANAPA, wala Tanzania Tourist Board. Tulichokiona pale ni Gapco, Tigo, TBL, Serengeti Breweries na kadhalika. Napenda pia Bunge lako Tukufu litambue theme iliyobeba mbio za marathon katika ku-promote Mlima Kilimanjaro ilikuwa; “Mbio zetu, Bia zetu.” Hapa ninahoji hivi kwa nini isingelitokea walau tunakuwa na theme inayosema “Mbio zetu, Utalii wetu”? Hizi ndizo t-shirt tulizovaa katika kongamano hili zenye ujumbe wa “Mbio zetu, Bia yetu.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu lilikuwa ni jambo la fedheha kuona Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana katika Wizara ya Habari anavalishwa t-shirt inayo promote Bia ya Kilimanjaro na siyo Mlima Kilimanjaro. Hii ni aibu kwa Wizara, aibu kwa Taifa na aibu kwa Mataifa yote yaliyoshiriki katika mbio hizi ambao walifika takribani 30, 000 katika mbio zile. Tulikuwa na watoto wadogo waliokimbia takribani 7,000, swali langu ni ujumbe gani tulioutoa kwa vijana hasa wadogo? Ni lini watafahamu umuhimu wa uwepo wa outo wa kivutio hiki muhimu katika Mkoa wa Kilimanjaro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa hoja yangu ni moja, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imejipangaje kutangaza vivutio vya nchi yetu kupitia olympic games itakayofanyika mwezi Agosti, 2016 nchini Brazil? Nchi yetu na hususan Wizara ya Maliasili na Utalii itueleze imejipangaje kutumia fursa za michezo katika kutangaza maliasili yetu katika olympic ya mwezi Agosti, 2016? Tanzania ni sehemu ya delegates watakaohudhuria olympic games, ambapo katika event hii tunatarajia tutakuwa na zaidi ya viewers three billion. Kwangu hii ni sehemu muhimu katika kutangaza maliasili yetu. Ningependa kupitia majibu ya karatasi kutoka kwa Waziri, nini mpango wa Serikali katika kutangaza maliasili ya Tanzania?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa Bungeni tuna half marathon ambapo Mheshimiwa Waziri Mkuu aliwahi ku-host event ya namna hii, Wabunge tumewahi kuwa sehemu ya ushiriki. Hapa nina hoja, je, Serikali kupitia Waziri mwenye dhamana, hatuoni umuhimu wa kutumia hata hizi platform za Ofisi ya Bunge katika ku-promote maliasili yetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hili nami napenda nimuombe Mheshimiwa Waziri kupitia ofisi yake aone na atambue umuhimu wa kutoa elimu ya kutosha kwa wafugaji, wakulima, na wadau wote katika sekta ya maliasili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, personally napenda niseme kuwa suala ka ecological system lina two key players; uoto wa maliasili, binadamu na shughuli zake hapa namaanisha shughuli za kilimo na ufugaji lakini katika wahusika hawa wawili binadamu katika utashi wake ndiye amepewa uwezo wa kuleta balance kati ya uoto wa maliasili pamoja na wanyama na suala zima za kilimo sasa hapa nilitaka niseme nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi maingiliano ya uoto wa maliasili na wanyama pamoja na wakulima ni binadamu pekee mwenye uwezo wa kuhifadhi maliasili ya Tanzania kwa ujumla wake. Kilimanjaro leo vivutio vya maporomoko ya maji yaani water falls yametoweka, mito imekauka; Mto Karanga Kikafu pamoja na Bwawa la Nyumba ya Mungu yote yameonesha dalili za nje, nje za kutoweka katika uso wa Tanzania kama wakazi wa Kilimanjaro bado wataendelea kuchoma misitu na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, ni ushauri wangu kwa Wizara husika kutoa elimu ya kutosha ili uoto wa asili uendelee kuwepo kwa vizazi na vizazi. Nchi ya Rwanda imekuwa ni role model kwa Tanzania na East Africa katika suala zima la uhifadhi wa mazingira, hapa tujiulize nini wastani wa wanyama kwa mfugaji mmoja mmoja? Nafikiri katika jibu tutakalolipata tutaweza kupiga hatua kutokea hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hitimisho langu pia ningependa niiombe Serikali yangu iweze kukumbuka royalties kwa wananchi wangu wa Mkoa wa Kilimanjaro kutokana na natural endowment tuliyonayo kwa Mkoa wa Kilimanjaro. Nasisitiza kwamba vijana wa Kilimanjaro wamebaki kuwa watazamaji, wahitimu wa vyuo vikuu wamebaki kuwa wabeba mizigo ya wazungu wanaokuja kupanda Mlima Kilimanjaro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kilimanjaro kama mikoa mingine nayo imekuwa ni sehemu ya wahanga katika suala zima la huduma za jamaii ilhali Mlima Kilimanjaro wenyewe na vivutio vyake vinachangia pato la sekta ya utalii kwa zaidi ya asilimia 34. Shule za Mkoa wa Kilimanjaro zina uhaba mkubwa wa matundu ya vyoo, katika shule za msingi na sekondari, hakuna madawati; zipo baadhi ya shule za msingi watoto wanakaa chini, vijana wengi wameingia kwenye mkumbo wa kuvuta bangi na dawa za kulevya. Hii yote ni kutokana na hali ya kukata tamaa baada ya kukosa ajira na kubaki na ajira ya vibarua vya wazungu/watalii katika nchi yetu. Naomba kuwasilisha.