Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema ambaye amenijalia kuiona jioni hii ya leo. Pia, nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kazi nzuri unayoifanya kusimamia Kanuni na Sheria za Uendeshaji wa Bunge. Mungu akutie nguvu na akupe afya ili uendelee kukalia Kiti hicho mpaka tunapomaliza Bunge hili la Bajeti, tarehe Mosi, Mwezi wa Saba. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mpango, Naibu Waziri wa Fedha na timu yao kwa kazi kubwa ambayo wameifanya katika kuandaa mpango huu wa Bajeti ya Mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hii iliyofanyika ni kubwa na hii kazi imefanywa na binadamu. Yamkini kukawepo na upungufu sehemu, lakini kwa sehemu kubwa, mambo makubwa yamefanyika na ambayo kwa hakika yanatupa dira na mwelekeo wa kuwa na Tanzania ya tofauti, Tanzania ya viwanda, Tanzania ya uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na eneo la maji na umwagiliaji, sehemu ambapo wachangiaji wengi waliotangulia kama si Wabunge wote wanagusia eneo hilo kwa sababu ndilo eneo ambalo sasa linamgusa kila Mtanzania na ndilo eneo ambalo lina kero kubwa kwa sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wamejitahidi sana katika kuweka bajeti kwa ajili ya kutekeleza miradi hii kama ambavyo hata wakati wa uwasilishaji wa Waziri wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji alisema kwamba, tunahitaji sasa kwa miaka mitano ijayo kuona ni namna gani ambavyo tunaweza tukamwondolea adha huyu mwana mama Mtanzania anayeishi kijijini kubeba ndoo ya maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili niseme bado ipo kazi kubwa ya kufanya na niungane mkono na waliotangulia kuchangia kwamba, katika kuondoa kero hii au tatizo hili, lazima tufanye maamuzi, sisemi kwamba, ni maamuzi magumu, lakini tuzingatie ushauri ule ambao kila mmoja anaposimama anajaribu kuutoa. Ili kuondoa kero hii, lazima tujibane na tutafute ni mahali gani ambapo tunaweza tukapata fedha kwa ajili ya kuongeza kwenye Mfuko huu wa Maji hususan maji vijijini na si kwingine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niungane mkono na waliotangulia kwamba tozo ya sh.i 50/= kwa kila lita kwenye mafuta, hebu tujaribu kufanya uamuzi huo tuipeleke kule ili tuongeze Mfuko huu na tuweze kutatua kero hii. Nasema hivi kwa sababu mifano iko hai, ukiangalia hata katika bajeti iliyotengwa nina uhakika kwa maka wa fedha 2016/2017, hata viporo ambavyo bado havijakamilika hatuwezi kuvikamilisha kwa bajeti hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano kwenye Jimbo langu la Ngara, kwa miradi ile ya vijiji 10 tu, mkataba ulikuwa ni bilioni tano nukta, mpaka sasa hivi Wakandarasi wameshalipwa bilioni mbili nukta sita, maana yake bado bilioni mbili nukta tano. Kwenye Bajeti hii, Fungu la Maji lililoenda kule ni bilioni mbili tu ambayo haitoshelezi hata kuwalipa Wakandarasi kama watamaliza miradi ile. Kwa maana hiyo, mwaka 2016/2017 hakuna miradi mingine itakayofanyika pamoja na kwamba kuna Kata nyingi ambazo zina tatizo la maji ikiwa ni pamoja na Mamlaka ya Mji Mdogo wa Ngara Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana nasema kwamba, lazima tuzingatie tuone ni namna gani tunavyoweza kuongeza kwenye Mfuko huu wa Maji hususan maji vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, kwa sababu kauli mbiu ni kuwa na Tanzania ya Viwanda, lazima kuwe na uzalishaji na uzalishaji huo unatoka mashambani na huko ndiko waliko Watanzania, wananchi walio wengi takribani asilimia 70, ambao wanafanya shughuli hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri hata Mheshimiwa Waziri mwenyewe kwenye hotuba yake ya Bajeti amekiri kwamba, hapo kuna changamoto kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna namna ambavyo tunaweza tukaleta mabadiliko ya viwanda kama hatutajikita na kuweka mikakati madhubuti ya kuongeza uzalishaji ili tuweze kulisha viwanda vyetu na ili tuongeze uzalishaji, ni lazima tuingie kwenye kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Jimbo langu kuna mabonde makubwa takribani hekta 5,000 na zaidi. Wizara ilishafanya survey ikaonekana yapo mabonde matano makubwa ambayo yakifanyiwa kilimo cha umwagiliaji yanaweza kubadilisha uchumi wa wana Ngara, lakini kuongeza pia pato la Taifa. Kwa sababu kundi hili linapokuwa maskini, linapokuwa halizalishi, maana yake halilipi kodi, kwa maana hiyo inazidi kuvuta hata wale wachache wanaolipa kodi, GDP ya Taifa inashuka kwa sababu ya kundi hili ambalo halijaangaliwa kwa umakini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mradi wa Bigombo - mradi wa umwagiliaji, ambao ulikuwa ukamilike tangu mwaka 2013. Mradi ule kama ungekuwa umekamilika ungeweza kuzalisha tani nyingi sana za mazao kutoka kwenye kilimo cha umwagiliaji, lakini kwenye Bajeti hii bado haikutengewa fedha pamoja na kwamba mradi ule umefikia kwenye asilimia 80. Badala yake zimetengwa bilioni karibu mbili kwa ajili ya mabonde mengine mawili kwa kufanya upembuzi yakinifu na detailed design kwa ajili ya kuja kuanzisha haya mabonde mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Mheshimiwa Waziri kwamba katika eneo hili, kwa sababu tayari lipo bonde ambalo mradi ulishaanza na uko kwenye asilimia 80 basi, kiasi cha fedha ambacho kimetengwa kwa ajili ya kwenda kwenye upembuzi yakinifu kwa mabonde mengine kiweze kuhamishiwa hapo ili kumalizia huo mradi na wananchi wa Ngara waweze kunufaika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Sheria ile ya Kodi, imejaribu kueleza juu ya kuondoa msamaha wa kodi hususan kwa ile Pay As You Earn kwa wafanyakazi. Ukijaribu kuangalia dhamira ya Serikali ni njema kuhakikisha kwamba, inapunguza ile kodi kutoka kwenye digit mbili na kubakia kwenye digit moja. Ukiangalia kwenye Bajeti hiiā€¦
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.