Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kusimama hapa nikiwa mwenye afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile, napenda kuipongeza Serikali yangu ya Awamu ya Tano kwa kasi iliyoanza nayo, imani yangu, Tanzania yetu iko kwenye mikono salama chini ya Serikali ya CCM. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizo, sasa naomba kujikita moja kwa moja kwenye michango yangu, ambapo nitaanza kuongelea suala la ajira kwa vijana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Serikali kwa juhudi inazochukuwa kuhakikisha vijana wanapatiwa ajira. Pamoja na jitihada hizi bado tunauhitaji mkubwa wa ajira kwa vijana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu kwa Serikali hizi milioni 50 ambazo zinatakiwa kwenda kwenye kila Kijiji zingetumika kuanzisha Community Bank katika kila Wilaya, ambayo vijana na makundi mengine yangeweza kukopa kwa masharti nafuu na kuweza kujiajiri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa niongelee issue ya elimu. Naipongeza Serikali kwa kuanzisha elimu bure hadi kidato cha nne. Huu ni mwanzo mzuri wa kuweza kuwajengea fursa sawa watoto wote nchini kwa kuwajengea uwezo. Naiomba Serikali iweze kwenda mbele zaidi hadi kidato cha sita kufanya kuwa elimu bure. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile, napenda kuishauri Serikali ione namna ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wanasoma Kada za Afya na nyingine ambazo tunahitaji sana kama Taifa mfano wa Kada hizo ni kama Kada ya Utabibu, Ukunga na kadhalika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa niongelee suala la kodi katika Sekta ya Utalii. Sekta ya Utalii inachangia asilimia 12 ya Pato la Serikali kwa Tanzania Bara na asilimia 27 kwa Tanzania Visiwani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, average ya Watalii kwa mwaka ni milioni moja na hii average imekuwa stagnant kwa zaidi ya miaka mitatu. Hii inatokana na Imposition ya kodi ambazo hazina tija katika Sekta hii. Ushauri wangu kwa Serikali iangalie upya hizi kodi na kuzifuta ili tuweze kuinua Utalii wetu kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitakuwa sijajitendea haki nisipoongelea issue ya CAG. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya PAC, naelewa umuhimu wa CAG naelewa kazi zake na naelewa umahiri wake. Wenzangu waliopita wameongelea sana kwa kirefu na kwa kina zaidi. Namwomba Waziri atakaposimama kwa ajili ya majumuisho atueleze ni jinsi gani atakavyoweza kupata fedha za kumwongeza CAG ili aweze kufanya kazi zake kwa umahiri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa leo sina michango mingi, naunga mkono hoja, ahsante!