Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JENISTA J. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Nina maombi maalum kama ifuatavyo:-
(i) Mgao wa madawati ufike Peramiho, kwa kuwa corridor hiyo inafika Muhukuru kutokea Tunduru kuvuka kuelekea Msumbiji;
(ii) Suala la upatikanaji wa teknolojia maalum kwa kuwezesha uwepo wa system ya vyoo Mlima Kilimanjaro ni muhimu sana kwa sasa;
(iii) Kwa kuwa sasa Serikali imeamua kukuza utalii kwenye sekta ya hoteli na huduma, ili kukuza ujuzi wahudumu wa sekta hiyo, kuna kila haja Wizara hii na Idara ya Kazi na Ajira zishirikiane kukuza ujuzi na kuondoa tatizo hilo haraka. Ofisi ya Waziri Mkuu imezindua mpango mkakati wa kukuza ajira; na
(iv) Kwa kuwa kuna malalamiko makubwa ya sekta ya upagazi katika kupandisha mizigo ya utalii Mlima Kilimanjaro, naomba masuala ya viwango vya kazi na ajira vilivyopo kisheria vizingatiwe katika kusimamia sekta hiyo.