Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri, Naibu Waziri na wataalamu wote chini ya Katibu Mkuu wa Wizara katika kipindi kifupi wameweza kufanya kazi ya kuwapa matumaini makubwa wananchi, ingawa matatizo ni mengi kwenye sekta ndani ya Wizara hii. Pamoja na yote tunapaswa kuwa na subira ya kujipanga na kuweka miundombinu ya mikakati ya kusafisha matatizo yaliyopo kwa kuyaweka katika kipaumbele ndani ya utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatana na hali halisi ya wananchi kuongezeka na ardhi/nchi ipo vilevile ni dhahiri haya mapori ya akiba 28 na mapori tengefu 42 yawezekana yamepotea au kupungukiwa sifa ya kuwa mapori ya akiba au mapori tengefu. Nashauri Serikali kufanya utafiti wa kukagua maeneo hayo na kupata idadi halisi ya uhalisia uliopo sasa na tupatiwe idadi na orodha yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, misitu tunaitumia wananchi katika shughuli mbalimbali na kuendelea kupungua kutokana na ukosefu wa nishati mbadala na kusababisha baadhi ya watumishi wa maliasili kuwa wasumbufu kwa wananchi wetu. Mazao ya misitu yamekuwa yanawanufaisha wachache na kukosesha mapato kwa Serikali. Ni vyema tukaweka mkakati wezeshi wa kupunguza usumbufu wa tozo zinazoingiliana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANAPA inajitahidi katika kujenga mahusiano mazuri na wananchi wetu, nashauri badala ya makusanyo yote kupelekwa kwenye Mfuko Mkuu, ni vyema wakabakiwa na hata asilimia 30 ili kuboresha shughuli wazifanyazo kwa wananchi wanaozunguka maeneo yao ya huduma za jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utalii una mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa. Mkoa wa Rukwa una vivutio kadhaa, mfano, Kalambo Falls. Tunahitaji vivutio vipitishwe na kutambuliwa na kufanyiwa matangazo, huku miundombinu ya kufikia kwenye eneo inafanyiwa kazi. Barabara ya kiwango cha lami (Matai – Kisumba – Mpombwe (Kapozwa) – Kalambo Falls) kwani eneo hilo linatumiwa zaidi na utalii wa Zambia kuliko Tanzania wenye eneo kubwa linalovutia katika kuyaona maporomoko hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kuona umuhimu wa kukuza utalii wa Nyanda za Juu Kusini (Rukwa), kubadilisha mwelekeo wa Mashariki na Kaskazini. Nchi hii pande zote kuna vivutio vya utalii. Naomba Waziri atuthibitishie vivutio vyetu vitatambuliwa lini ili watalii wafike na tuongeze Pato la Taifa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha na kuunga mkono hoja.