Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuwapongeza Mawaziri wa Wizara hii nyeti kwa uchumi wa nchi yetu. Kwa kuzingatia unyeti wa Wizara hii naomba kuchangia yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni Makumbusho ya Taifa, kumekuwa na tatizo la muda mrefu kwa watumishi wa Makumbusho ya Taifa kutopandishwa vyeo. Hali hii inakatisha moyo sana kwa wafanyakazi wengi kuhamia taasisi nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya waajiriwa wapya wanapogundua Makumbusho hawatoi vipaumbele kwa wafanyakazi wake wanaamua kuacha kazi. Shirika la Makumbusho ya Taifa ni muhimu katika kuhifadhi mambo yanayoshamiriwa na jamii na ambayo yanapotea kwa kasi sana, lakini Wizara haiipi kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imetegemea zaidi kwa wanyamapori na tangu Waziri na Katibu Mkuu wateuliwe hakuna aliyefika Makumbusho. Nyumba haitoshi Makumbusho ya Posta kumbi mbili zimefungwa, ukumbi wa baiolojia na wa mila na desturi umefungwa kwa zaidi ya mwaka sasa.
Naomba suala hili lifanyiwe kazi na Makumbusho ya Taifa ipewe kipaumbele katika bajeti hii ili kuyapa uhai. Vilevile kuongeza motisha kwa wafanyakazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kimondo Wilayani Mbozi. Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe kuna kimondo ambacho kilianguka, kimekuwa kikitembelewa na Watanzania kutoka pande zote za nchi yetu na vilevile wasanii kutoka nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishauri Serikali iangalie namna nzuri ya kuboresha mazingira ya kile kimondo. Mazingira yale yakiboreshwa na vilevile kimondo kile kikipewa kipaumbele na Wizara katika kutangazwa kitaweza kujulikana Kimataifa na hivyo Taifa litaweza kujiingiza kipato huku wakazi wa Mbozi wakinufaika kiuchumi na kijamii na uwepo wa kivutio hicho katika Wilaya yao na Mkoa wa Songwe kiujumla.