Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Naishauri Serikali, Sheria za Ardhi na Sheria za Uhifadhi, kwa maana ya mipaka inayohusiana na maeneo ya maliasili itazamwe upya kwa lengo la kuondoa migogoro na migongano kati ya wananchi na maliasili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha wataalam wa ardhi, maliasili, kilimo na maji wakutane ili kuisaidia Serikali kumaliza migongano na migogoro ya ardhi kwa kuifanyia uchambuzi wa kina na hatimaye watoe mapendekezo kwa Serikali ili yaweze kupitiwa na kufanyiwa kazi, bila hivyo migogoro hii haitaondoka au haitakwisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mifugo kuingizwa kwenye hifadhi na hifadhi kufanywa malisho halikubaliki. Kuachia jambo hili liendelee litasababisha uharibifu mkubwa wa ardhi, mazingira, kuondoa uoto wa asili kutokana na ng‟ombe kukanyaga hovyo. Misitu itakwisha kwani wafugaji ndio wanaokata miti na kuchoma moto kwa lengo la kutaka nyasi ziote upya kwa ajili ya malisho yao, maliasili itatoweka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la majangili, askari wa wanyamapori waendelee kupatiwa mafunzo na mbinu zitakazowawezesha kukabiliana na majangili. Aidha, vitendea kazi ni lazima vipatikane kwa askari hawa, bila kufanya hivyo kuhimili vishindo vya majangili itakuwa ngumu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kuboresha miundombinu itakayowezesha watalii kutembelea hifadhi kwa urahisi zaidi na kuingizia mapato ya Serikali kwa wingi.