Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri. Mchango wangu upo kwenye suala zima la utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Lushoto kuna vivutio vingi vya kitalii lakini vivutio vile havichangii Pato lolote la Taifa letu kwa sababu utalii ule unafanywa kienyeji. Hivyo basi niombe Serikali ifungue chuo cha kitalii Lushoto ili vijana wetu wapate elimu ya utalii ili wasiendelee kufanya kazi ile kienyeji na kuisababishia Serikali kukosa mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niishauri Serikali, yale maeneo yote yenye vivutio yatengenezwe ili watu wasiingie kiholela, ikiwezekana kuwe na vizuizi. Niombe Serikali yangu Tukufu iwaangalie hawa watu wanaovuna mti mmoja mmoja, waweze kuchana mbao zao kwa kutumia chainsaw kwani wakulima hawa hawana uwezo wa kununua mashine za kuchana mbao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hayo walikuwa wanatumia misumeno ya mikono ambayo hakuna watu wanaoitumia kwa sasa maana walikuwa wanatumia wazee na wazee wengi wameshakufa na waliobaki wamezeeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii pia imepelekea baadhi ya watu ambao hawana nia nzuri hasa polisi wanawakamata sana watu wanaokata miti kwa chainsaw, na askari hawa wameacha kufanya kazi zao nyingine, kazi yao kusikiliza maeneo yanayolia chainsaw ili wakakamate.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la asilimia 20 kumekuwa na tabia ya Maafisa Misitu kuchukua asilimia hizo hata kama mtu anavuna mti wake kwa matumizi yake binafsi. Niombe Serikali yangu iwape Wabunge zile sheria za misitu ili Wabunge tukawaelimishe wakulima wetu wa miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengi yaliyozungukwa na misitu mameneja hawatoi mgao kwa vijiji vilivyozunguka msitu pamoja na vikundi vya kina mama wajane, vijana pamoja na vikundi vya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu, hasa katika Wilaya ya Lushoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niendelee kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Mungu amlinde na kumzidishia umri pamoja na kumpa afya nzuri.