Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko makubwa naomba kuchangia mawazo yangu baada ya kupitia kitabu cha hotuba ya Wizara ya Maliasili na utalii. Nimesikitishwa sana kuona hotuba yenye kurasa zisizopungua 120 kutoelezea vizuri mipango na mikakati ya sekta ya utalii Zanzibar. Sote tunajua contribution ya Zanzibar kwenye sekta hii ya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Wizara yako inajitihada za makusudi katika kuhakikisha utalii wa Zanzibar unainuka na unatambulika zaidi duniani, ila kiukweli wazawa hawafaidiki ipasavyo. Inasikitisha kuona hata mpishi wa hoteli ni foreigner, sitaki kuamini kwamba wazawa hawana elimu ya kutosha ku-operate hoteli na sehemu nyingi za kitalii. Ni kwa nini Wizara isichukue juhudi za kuboresha mitaala katika vyuo vyetu vya utalii vilivyo ndani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama sitapata maelezo mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wakati wa ku-wind-up nakusudia kushika mshahara wa Mheshimiwa Waziri.