Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema jambo moja, tulipopata Uhuru mwaka 1961 tulisema na tuli-declare wazi kwamba nchi yetu ni nchi ya wafanyakazi na wakulima. Hii ndiyo ilikuwa kauli na ndiyo iliyotengeneza direction ya nchi yetu, wafanyakazi wakawa na vyama vya wafanyakazi, wakulima wakawa na ushirika na Serikali ikaweka nguvu katika kutunga sheria, kutengeneza sera ambazo zingeweza kuwajengea mazingira bora wakulima na wafanyakazi wa nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya 1990 tukafanya liberalization tukatambua kundi la tatu katika nchi yetu, kundi la wafanyabiashara tukawapa heshima kubwa na kuwaita wawekezaji, tukawatengenezea sera, tukawatengenezea sheria ili kuwajengea mazingira ya wao kufanya biashara. Mpaka leo kama nchi hatujawahi kuwa na deliberate move ya kuweza kuli-accommodate kundi kubwa linaloitwa la wafugaji. Huko nyuma tumekuwa tukisema kwamba nchi hii ni yetu sote, sungura mdogo tutagawana wote. Nataka niseme leo, Mwalimu Nyerere aliwahi kuongea mwaka 1975 na wafanyakazi, akiwaambia wafanyakazi utii ukizidi unakuwa uoga, na siku zote uoga huzaa unafiki na unafiki huzaa kujipendekeza na hivyo kuzaa mauti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwalimu aliendelea kuwaambia wafanyakazi, kama ninyi watumishi wa umma kwa wingi wenu mmeshindwa kupiga kura ya kuwaondoa viongozi dhalimu ni bora mfe. Na mimi nasema sisi kama CCM kwa wingi wetu tunashindwa kuishauri Serikali kwa ukweli hatuna sababu ya kubaki kuwa madarakani. Nayasema haya kwa moyo mweupe, nikiwa mwanachama wa chama chetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi. Hili ni jukumu letu Serikali ya Chama cha Mapinduzi kutafuta suluhisho la migogoro ya wakulima na wafugaji na hili siyo jukumu la Waziri peke yake ni jukumu letu sote kama chama na kama Serikali. Hili siyo jukumu la Mheshimiwa Maghembe, hili ni jukumu la Waziri wa TAMISEMI, Waziri wa Kilimo, Waziri wa Ardhi, Waziri wa Katiba na Sheria ili tuweze kutengeneza mazingira bora kwa ajili ya wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuambie leo hii kaka yangu Mheshimiwa Kakunda yule pale, katika Wilaya ya Sikonge over 70 percent ni hifadhi, hawa wananchi wakulima na wafugaji wanaenda wapi? Mkoa wa Tabora Pori la Ipala linaanzia Nzega linaenda Uyui, linaenda Tabora Manispaa, linaenda Sikonge, hakuna maeneo. Wakulima wetu na wafugaji wetu wanakwenda wapi? Lazima ufike wakati na ningemuomba Waziri wakati unakuja kufanya wind up hapa useme clearly kwamba tarehe 15 mfugaji hatotolewa porini bila kumuandalia maeneo. Maana yake mkimtoa porini mnaenda kumchonganisha na ndugu yake mkulima waanze kuumizana, hili ni jambo la kwanza. (Makofi)
Mheshimwia Mwenyekiti, kwa hiyo ndugu zangu, dhambi hii na Bunge liiagize Serikali, Bunge la Oktoba wanapokuja hapa kama Serikali waje wametoa affirmative action juu ya tatizo la wafugaji na wakulima. Nataka niwape mfano, mwaka 2006 wafugaji waliondolewa Ihefu wakapelekwa tena Mheshimiwa Abdallah Ulega alikuwa DC yule pale, mnampeleka mfugaji eneo la kijiji hamjamwekea miundombinu. Bajeti ya mwaka huu Mheshimiwa Mwigulu hana fedha ya kuchimba hata mabwawa mawili na tumeipitisha hapa, tunataka kwenda kusaidia matatizo ya wafugaji na wakulima hatuwezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuiombe Serikali ije na affirmative action na solution ya jambo hili ili tuondoke kwenye mgogoro huu iwe ni leo, ni kesho, kwa kizazi cha watoto wetu na wajukuu zetu huko mbele. Inawezekana hatupendi kuyasikia, lakini ndiyo ukweli wa jambo hili. (Makofi)
Mheshimiwa mwenyekiti, jambo la pili, siongelei wafugaji na wakulima tena. Jambo la pili leo maliasili ukitazama takwimu zilizotolewa na World Travel Tourism Council on Economic Impact in Tanzania ya mwaka 2015, inasema maliasili yaani utalii ume-create ajira mwaka 2014 watu 1,300,000. Wana-project mwaka 2025 watu watakaokuwa wameajiriwa katika sekta hii direct or indirect ni 1.6 million, growth ya 2.7 percent. Lakini investment lile kapu la uwekezaji kutoka nje na ndani kwa mwaka 2014 uwekezaji uliyofanywa katika sekta ya utalii ni trilioni 1.8. Wana-project mwaka 2025 utakuwa 3.7 ambao ni 9.8 growth ya 0.3 percent.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mheshimiwa Ally Saleh kaka yangu kaongea mambo ya msingi sana. Tunasema tuangalie emerging economics kwa ajili ya uwekezaji, kwa ajili ya ku-attract watalii, swali la kujiuliza ripoti za dunia zinasema uchumi wa dunia kuna slow growth. Nimeisoma hotuba ya Mheshimiwa Profesa, hakuna plan iliyo-accomodate kuwepo kwa kushuka kwa uchumi wa dunia kwa 0.0 percent namna gani utaathiri Utalii wetu wa ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma kitabu alichokiandika kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango, anakiri Southern part and Western part of this country tourism haiwezi kukua kwa sababu ya infrastructure mbovu. Tunafanya nini kama Serikali? Mbali na hapo hunting (uwindaji) na Serikali ilipitisha katika Bunge lililopita kuwasaidia locals wawekeze katika uwindaji, kati ya vitalu 160 walivyopewa wawindaji, vitalu 50 vimerudishwa Serikalini kwa sababu gharama ya leseni, ushuru ni kubwa mno. One of expensive destination duniani ni Tanzania, eneo lingine hata landing rate za kutua kwenye viwanja vyetu vya ndege ni kubwa watalii wanatua Kenya ndiyo wanakuja Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeiomba Serikali iende ikafanye review upya, itazame upya sekta hii ya utalii kwa kuangalia variables zote za dunia, waje na mpango ambao kama watahitaji idhini ya Bunge tuwasaidie, bila ya hivyo growth kwenye sekta ya utalii ukiitazama kwa miaka mitano ijayo mpaka kumi ni 2.5 percent peke yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo...
MWENYEKITI: Ahsante.